WAENDESHA BODABODA KUINULIWA KIUCHUMI KWA KUKOPESHWA BODABODA YENYE BIMA KUBWA NA MKOPO BILA RIBA WALA DHAMANA



Mrisho Gambo's photo.
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akiongea na waendesha boda boda wa jiji la Arusha ambapo alisema kuwa nimefanya kikao na vijana wa Bodaboda Jiji la Arusha. Tunawaandalia utaratibu mzuri wa kujikwamua kiuchumi. Tumewatafutia pikipiki 200(zenye thamani ya Million 400 ) ambazo tutawagawia bila riba wala dhamana. Badala ya kupeleka pesa kwa tajiri watapelekea kwenye mfuko wao na ikitimia pesa ya pikipiki ,  hiyo inakuwa Mali yake na tuna nunua pikipiki nyingine na kumpa kijana mwingine. Pia tumezikatia BIMA kubwa na Mbunge wa Viti maalum (Mhe Catherine Magige) atawalipia bima ya afya kaya zote 200. Pia tutawapatia mafunzo. Uongozi unao acha alama. picha na Mahmoud Ahmad Arusha.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni