WAFANYAKAZI 66 WAPUNGUZWA KAZI HALMASHAURI YA JIJI LA ARUSHA

Image result for kihamia mkurugenzi jiji la arusha 

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji La Arusha Athmani Kihamia ametangaza kusitisha mikataba ya wafanyakazi 66 kati ya 132 wasio na kazi za ulazima katika halmashauri hiyo ,lengo likiwa ni kubana matumizi, ambapo fedha zitakazookolewa zitaelekezwa kwenye matumizi ya miradi ya maendeleo na ulipaji wa madeni ya nyuma.

Alisema hayo wakati akiongea na wanahabari ofisini kwake ambapo alisema kuwa kabla hapo alikuwa akilipa mishahara ambayo ilikuwa inaibebesha halmashauri hiyo mzigo mkubwa na kufanya ielemewe kwa kupoteza fedha hizo ambazo zingetumika kwenye miradi ya maendeleo na ulipaji wa madeni.

Alisema kuwa anasimamia kubana matumizi ili kulipa madeni yenye kero na tija kama  ambavyo walielekezwa na kamati za bunge na mdhibiti mkuu wa serikali(CAG) kuhakikisha wanabana matumizi yasiyo na ulazima ili kulipa madeni ya muda mrefu.


“Wafanyakazi hao 132 ambao walikuwa kwenye  vitengo mbali mbali ndani ya halmashauri hiyo kati yao 66 ndio tumewapunguza kwa kuwa kazi zao hazina umuhimu na wamekuwa mzigo hivyo ni busara kuwapunguza kuhakikisha tunabana matumizi na kulipa madeni ya halmashauri ya nyuma”alisema Kihamia.

Akizungumzia tuhuma za ulipaji wa fedha za walimu 701 kiasi cha tsh. million 169 zikiwa madeni ya walimu ambazo hazikufuata utaraatibu wa kuidhinishwa na baraza la madiwani au kamati ya fedha na uchumi alisema kuwa fedha hizo zinatokana na mapato ya ndani nasi lazima fedha zinazotumika kuidhinishwa na baraza au kamati ya fedha.

“Kumekuwa na tuhuma mbali mbali za fedha za madeni ya waalimu kutoka kwa madiwani  wetu, fedha tulizowalipa waalimu kiasi cha million 169  kati ya walimu 701 hizi fedha mchakato wake ni fedha za mapato ya ndani hazihitaji mpaka kuwepo na ukaaji wa vikao vya baraza wala kamati”alisisitiza Kihamia.

Akawataka wale wanaolifanya suala hilo kisiasa zaidi sio kweli kwani yeye anafuata kanuni na taratibu katika ulipaji wa madeni ya fedha za watumishi wa umma kama alivyowalipa walimu hao.

Akatanabaisha kuwa katika kuhakikisha suala zima la upatikanaji wa huduma bora za Afya halmashauri hiyo imenunua Genereta kubwa katika kituo cha Afya Levolosi ikitumia mapato yake ya ndani jambo ambalo limerahisha utoaji wa huduma pindi umeme unapokatika.

Aidha halmashauri hiyo imeagiza vifaa vya kisasa vya upimaji wa ardhi vitavyosaidia kuondokana na migogoro ya mipaka kwa wakazi na hivyo kuweza kuwapimia Ardhi wakazi wote wa halmashauri hiyo ambao maeneo yao mengi hayajapimiwa hadi sasa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni