MAAFISA WANOLEWA KUDHIBITI UTOROSHWAJI WA ,MAGOGO MIPAKANI

magogo
Shirika la uhifadhi wa maliasili na mazingira Duniani(WWF)kwa kushirikiana na wakala wa misitu Tanzania(TFS) wamefanya mafunzo kwa maofisa misitu waliopo mipakani na maafisa Kilimo pamoja na idara ya forodha kwa lengo la kudhibiti utoroshwaji wa mazao ya misitu katika mipaka inayotenganisha nchi na 
nchi.

Semina hiyo ya siku tatu inayofanyika jijini Arusha na kuzishrikisha nchi nchi Tatu Tanzania,Kenya,Uganda na Zanzibar imelenga kuwapatia elimu ya uelewa maafisa hao ilikutambua thamani ya mazao ya misitu na maliasili yanayopitishwa mipakani hususani mbao ambazo zimekuwa zikitoroshwa yakiwemo pia magogo.

Akizungumza katika semina hiyo Mratibu wa mpango ya misitu Isaack Malugu alisema kuwa Hatua hiyo itazisaidia nchi hizo kuokoa mamilion ya fedha yalikuwa yakipotea kutokana na kutokuwa na uelewa wa thamani ya mazao ya misitu.

Malugu alitaja baadhi ya mipaka ambayo imekuwa vinara wa kuvusha mazao ya misitu ikiwemo mkaa kuwa ni pamoja na mpaka wa NamangaArusha,Hororo Tanga na Taveta Kilimanjaro,ambapo alitolea mfano wa mpaka wa hororo kuwa kiasi cha dola million kumi zimekuwa zikipotea kila mwaka

“Kuna Baadhi ya miti hairuhusiwi kuvushwa bila kibali maalumu ambapo pia katika usafirishaji kuna baadhi ya magari yamekuwa yakichanganya mbao na magogo yenye thamini kubwa kama mloliondo mpingo na msindawe ambayo inathamani kubwa na haivunwi bila kibali maalumu”alisisitiza Magulu

Kwa Upande wake Ismail Aloo kutoka wakala wa misitu Tanzania alisema kuwa mafunzo hayo yataenda sambamba na kuwajengea uelewa maofisa kutoka idara za forodha kwenye mipaka ambapo wataweza kudhibiti mazao wa misitu kwa kutambua aina za miti inayopita mipakani.

Alisema kuwa hii itasaidia kudhibiti mazao ya misitu na maliasili katika mipaka yetu na kujua thamani na kujua sheria za nchi zinazopakana nazo sheria zao zinasemaje katika suala zima la mazao ya misitu huku serikali ikipata mapato yake halali.

Pia itasaidia uadilifu kwa wafanyakazi ambapo imekuwa changamoto kubwa katika usimamizi wa mazao ya misitu hapa nchini hali inayopelekea upotevu wa mapato na kushindwa kukadiria ipasavyo mazao hayo ya misitu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni