SERIKALI YATAKIWA KUTOLEA MACHO SUALA ZIMA LA TABIANCHI

Image result for climatechange
Na Mahmoud Ahmad Arusha
Serikali imetakiwa kulipa kipaumbele suala zima la Mabadiliko ya Tabia nchi ambapo imeonekana shughuli za kibinadamu zimakuwa zikiathiri mazingira kwa sehemu kubwa hapa nchini inayopelekea mabadiliko ya Tabianchi na ongezeko la joto.

Akitoa Mada kwenye semina ya Waandishi wa Habari iliyoandaliwa na Oakios Tanzania Mkurugenzi wa Taasisi ya Carbon Tanzania Jo Anderson alisema kuwa shughuli za kibinadamu hapa nchi zimakuwa ndio sababu kubwa ya ongezeko la Joto linalopelekea Mbadiliko ya Tabianchi.

Alisema kuwa Maeneo mengi ya vijijini ndio yameathirika ikiwemo ukataji wa kuni na uharibifu wa vyanzo vya maji pamoja na matumizi ya kilimo katika kubadilisha matumizi ya misitu kwenda kwenye kilimo.

Alisema kuwa Wandishi wa habari wamekuwa wakipata changamto kubwa kuandika habari za kisayansi na hivyo kujikuta wakiwa hawana uelewa mkubwa kwenye masuala hayo kitaaluma ambapo semina hiyo itawapa mwanga kuhusiana na mabadiliko ya Tabianchi katika kuandika habari zao.

“Shughuli za kibinadamu zimakuwa ndio changamoto kubwa ya mabadiliko ya Tabianchi ambapo uharibifu wa mazingira kwa ukataji miti na uharibifu wa vyanzo vya maji,na Ardhi kunakoenda sambamba na uharibifu wa misitu”alisisitiza Anderson.

Kwa upande wake Maratibu wa semina hiyo Silvia Ceppi alisema kuwa semina hiyo ya siku moja kwa wanahabari ni kuwapa uelewa wa masuala mazima ya kisanyansi kujua mabadiliko ya tabianci katika kuboresha taarifa zao wanazoripoti kila siku juu ya kadhia hiyo.

Alisema kuwa uzalishaji wa gesi joto kunakofanywa na mataifa yenye viwanda humu duniani ndio sababu kubwa ya uharibifu wa mazingira na kuwapa changamoto kubwa ya kuandaa mikakati ya uthibiti wake na hivyo kuiomba serikali kutupia macho masuala ya uharibifu wa mazingira na ongezeko la joto hapa nchini.
Mwisho……………………………………………………………

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni