LIVERPOOL YAENDELEZA MAKALI KWA KUICHAKAZA HULL CITY MAGOLI 5-1

Timu ya Liverpool imeibuka na ushindi wa magoli 5-1 dhidi ya Hull City katika mchezo wa Ligi Kuu ya Uingereza ulioshuhudia Ahmed Elmohamady akitolewa nje kwa kadi nyekundu na kuiathiri Hull.

Katika mchezo huo Liverpool walikuwa wa kwanza kufunga goli kupitia kwa Adam Lallana na kuachia shuti lililotinga kwenye eneo la juu la kona ya goli, kisha James Milner akifunga la pili kwa penati baada ya Elmohamady kucheza rafu na kupewa kadi nyekundu.
Sadio Mane aliongezea goli la tatu akimalizia vyema kazi nzuri ya Lallana, huku Hull wakichomoa goli moja kupitia David Meyler. Philippe Coutinho aliongeza la nne na kisha James Milner kufunga kwa penati la tano baada ya Daniel Sturridge kuangushwa.
                                 James Milner akiifungia Liverpool goli kwa mkwaju wa penati
                 Mpira uliopigwa na Philippe Coutinho ukielekea kutinga wavuni na kuandika goli

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni