WATU LAKI NNE HUFA KILA MWAKA DUNIANI KUTOKANA NA KUKAA MUDA MREFU


Utafiti uliofanywa na wataalam wa afya wa nchini Marekani umeonyesha kuwa watu wapatao 1,200 hufariki dunia kila siku duniani kutokana na kukaa kwa zaidi ya muda wa saa tatu.

Ingawa kukaa ni sehemu ya maisha, lakini takwimu zinaonyesha vifo vya 433,000 hutokea kila mwaka duniani kutokana na hulka ya kukaa kwa masaa mengi.

Vifo vitokanavyo na mtu kukaa kwa muda mrefu vinachangiwa na kutokuwa na usawa wa uzalishaji na uharibifu wa molekuli za mwilini zisizo imara ambazo huweza kusababisha kifo.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni