WANAWAKE WANNE WAUWAWA KWA KUPIGWA RISASI NCHINI MAREKANI

Wanawake wanne wapigwa risasi na kufa na mwanaume mmoja amejeruhiwa vibaya katika eneo la maduka huko Burlington, katika jimbo la Washington nchini Marekani.

Polisi wametoa picha ya mtu anayetuhimiwa kufanya tukio hilo ambaye aliondoka kwenye eneo la tukio akiwa na bunduki aina ya rifle.

Jengo la duka la The Cascade Mall pamoja na maduka ya karibu watu wameondolewa na polisi wamewataka wananchi kukaa mbali. Bado haijafahamika sababu ya shambulio hilo.

Mtuhumiwa ameelezwa kuwa ni mwanaume mwenye asili ya Hispania na alionekana akielekea njia ya magari ya Interstate 5.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni