Naibu
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akikata tiketi
 ya mabasi ya Mradi wa Mabasi ya Mwendo Kasi ya UDA-RT katika Kituo cha 
Ubungo jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kusafiri na mabasi hayo kutoka 
katika kituo hicho kuelekea Posta. Kushoto ni Mkuu wa Kikosi cha Usalama
 Barabarani nchini, Naibu Kamishna, Mohamed Mpinga naye akiwa mmoja wa 
wasafiri wa mabasi hayo. Masauni aliyapanda basi la Mwendo kasi mara 
baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika Stendi Kuu ya Mabasi Ubungo 
kukagua mabasi mabovu pamoja na usalama wa abiria. Picha zote na Wizara 
ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

 
Naibu
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akiigusisha 
tiketi yake katika mashine ya Mradi wa Mabasi ya Mwendo Kasi ya UDA-RT 
katika Kituo cha Ubungo jijini Dar es Salaam ili mruhusu kuingia ndani 
ya stendi hiyo kwa ajili ya kusafiri na mabasi hayo kutoka katika kituo 
hicho kuelekea Posta. Mara baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika 
Stendi Kuu ya Mabasi Ubungo kukagua mabasi mabovu pamoja na usalama wa 
abiria Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Naibu
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akiingia ndani
 ya Basi la Mradi wa Mabasi ya Mwendo Kasi ya UDA-RT katika Kituo cha 
Ubungo jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kusafiri na basi hilo kuelekea 
katikati ya Jiji, baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika Stendi Kuu
 ya Mabasi Ubungo kukagua mabasi mabovu pamoja na usalama wa abiria. 
Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Naibu
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni  akiwa ndani 
ya moja ya mabasi ya mradi wa mabasi ya mwendo kasi ya UDA-RT jijini Dar
 es Salaam akitoka kituo cha Ubungo kuelekea katikati ya Jiji, baada ya 
kufanya ziara ya kushtukiza katika Stendi Kuu ya Mabasi Ubungo kukagua 
mabasi mabovu pamoja na usalama wa abiria. Picha na Wizara ya Mambo ya 
Ndani ya Nchi.
Naibu
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni  akitelemka 
katika moja ya mabasi ya mradi wa mabasi ya mwendo kasi ya UDA-RT jijini
 Dar es Salaam katika kituo cha Nyerere, Posta. Masauni alipanda basi 
hilo akitokea Ubungo baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika Stendi 
Kuu ya Mabasi Ubungo kukagua mabasi mabovu pamoja na usalama wa abiria. 
Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Naibu
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni  akiondoka 
katika Kituo cha Mabasi ya Mwendokasi cha Nyerere, Posta, mara baada ya 
kusafiri na usafiri huo akitokea Ubungo, jijini Dar es Salaam, baada ya 
kufanya ziara ya kushtukiza katika Stendi Kuu ya Mabasi Ubungo kukagua 
mabasi mabovu pamoja na usalama wa abiria. Katikati ni Mkuu wa Kikosi 
cha Usalama Barabarani nchini, Naibu Kamishna, Mohamed Mpinga Picha zote
 na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. 
 
                                                                                                     Felix Mwagara, MOHA 
NAIBU
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ameupongeza 
Mradi wa Mabasi ya Mwendo Kasi ya UDA-RT wa jijini Dar es Salaam na 
kuwataka wananchi waendelee kuyatumia mabasi hayo wanaposafiri sehemu 
mbalimbali jijini humo. 
Mhandisi Masauni ameyasema hayo jana 
mara baada ya kusafiri na mabasi hayo kutoka kituo cha mabasi hayo cha 
Ubungo mpaka katikati ya jiji kwa lengo la kujionea jinsi mabasi hayo ya
 mwendokasi yanavyohudumia abiria pamoja na kuwapa moyo wananchi kuwa 
usafiri huo unatumiwa na mwananchi wa aina yeyote. 
Akizungumzia 
usafiri huo, Masauni alisema mradi huo umerahisisha sana usafiri kwani 
ametumia dakika chake akitokea Ubungo hadi Posta katikati ya jiji bila 
usumbufu wowote, hivyo mradi huo ameomba uendelee kulindwa pamoja na 
kutunzwa na UDA-RT na wananchi wenyewe kwa ujumla. 
“Mimi kwa 
kweli nimeufurahia sana usafiri huu, Serikali imefanya jambo kubwa sana 
kwa wananchi wake, kwa kuwajali wananchi kwa kuuleta mradi huu ambao 
unarahisisha safari kwa uharaka zaidi na pia unapendezesha jiji kwa 
jinsi magari yalivyo nadhifu,” alisema Masauni ambaye pia alilipa nauli 
kwa kupanga foleni kama wananchi wengine wanavyofanya wanapotaka 
kusafiri na usafiri huo. 
Masauni aliongeza kuwa; “Nimefarijika 
sana na lugha ya adabu na tulivu ambayo wanaitumia madereva wa mabasi 
hayo wanapowatangazia wananchi vituo mbalimbali vya kushuka na kuingia 
kwenye mabasi hayo, hii inasaidia kuwa na mawasiliano mazuri na abiria, 
pia inaonesha madereva hao wamefunzwa vizuri na wanaipenda kazi yao.” 
Hata
 hivyo, Masauni alitoa ushauri kwa uongozi wa mabasi hayo, kuruhusu 
wananchi waingie ndani ya mabasi hayo kwa idadi ambayo haitaleta kero 
kwa abiria wengine ili kupunguza wingi wa abiria hao kwa lengo la 
kuepuka mbanano mkubwa wa abiria. 
Pia aliwataka wananchi wa jiji
 hilo kuyatunza mabasi hayo, na pia kukubali maelekezo ya madereva 
wanapotoa matangazo wanapokuwa safarini kuelekea maeneo mbalimbali ya 
jiji. 
Naibu Waziri huyo alipanda mabasi hayo akitokea Ubungo 
mara baada ya kumaliza ziara yake ya kushtukiza kwa kutembelea Stendi 
Kuu ya Mabasi Ubungo kwa lengo la kukagua mabasi mabovu pamoja na 
usalama wa abiria wanaosafiri na mabasi hayo.  Masauni pia alifanya 
ziara hiyo ya ghafla kwa kutembelea Stendi ya Kibaha, mkoani Pwani. 
 
 
 
 
  
 
 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni