Balozi
 Liberata Mulamula akiwasili nje ya jengo lenye studio ya Kilimanjaro 
tayari kuongea LIVE katika kipindi cha Jukwaa langu kinachorushwa kila 
siku ya Jumatatu kuanzia saa 12 jioni mpaka saa 2 usiku saa za Mashariki
 za Marekanui. anayemfungulia mlango ni Abdul Malik
 Balozi
 Liberata Mulamula akiingia ndani ya studio akiwa amesindikizwa Harriet 
Shangarai (kushoto) ambaye pia ni Mkurugenzi wa studio hiyo, kulia ni 
Afisa Ubalozi Swahiba Mdeme na Abdul Malik
 Balozi
 Liberata Mulamula akipata maelezo kutoka kwa studio meneja ambaye pia 
ni mtangazaji na mtayarishaji wa kipindi cha Jukwaa langu, Bwn. Mubelwa 
Bandio (hayupo pichani) Kushoto ni Afisa Ubalozi Swahiba Mdeme 
akifuatilia maelezo hayo.
 Mhe.
 Liberata Mulamula akiendelea kusikiliza maelezo kutoka kwa meneja wa 
studio Mubelwa Bandio ambaye ni mtangazaji na mtayarishaji wa kipindi 
cha jukwaa lako. Kati ni matangazaji maarufu wa Radio ya Times FM na 
aliyewahi kutangaza  Radio One Bi. Rose Chitalah ambaye pia anamsaidia 
Mubelwa Bandio katika utangazaji na kuchangia hoja mbalimbali katika 
kipindi cha Jukwaa langu.
 Balozi
 Liberata Mulamula akiendelea kujibu maswali ya watangazaji mahiri 
Mubelwa Bandio (kulia) na Rose Chitalah (hayupo pichani ) na 
wasikilizaji waliokua na shahuku ya kumuuliza maswali.
 
 Balozi Liberata Mulamula akiendelea kujibu maswali ya watangazaji 
mahiri Bwn. Mubelwa Bandio (hayupo pichani ) na Rose Chitalah (kushoto)
 Kutoka
 kushoto ni Afisa Ubalozi Swahiba Mdeme, Mhe. Balozi Liberata Mulamula 
na mtangazaji mahiri Rose Chitalah wakiwa katika picha ya pamoja.
 Kutoka
 kushoto ni Dj Luke Joe, Meneja wa studio ya Kilimanjaro,  Mubelwa 
Bandio, Mhe. Balozi Liberata Mulamula na mtangazaji mahiri Rose Chitalah
 wakipata picha ya kumbu kumbu na Balozi Liberata Mulamula anayemaliza 
muda wake kama Balozi wa Tanzania nchini Marejkani na Canada na sasa ni 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni