Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Arusha Onesmo  Ole
 Nangole kulia akizungumza na waandishi wa habari leo mara baada ya 
kuhamia rasmi chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA)kushoto ni Katibu Mwenezi wa CCM mkoa wa Arusha Isaac Joseph Maarufu kama Kadogoo(Habari Picha na Pamela Mollel wa jamiiblog)
Katika hali isiyokuwa ya kawaida Chama cha Mapinduzi kimeendelea kupoteza  wanachama  wake mara baada  Mwenyekiti
 wa chama hicho Mkoa wa Arusha, Onesmo Nangole pamoja na Katibu Mwenezi 
wa Mkoa huo Isaac Joseph kutangaza rasmi kukihama chama hicho cha CCM na
 kujiunga na CHADEMA.
Uamuzi
 huo ulifanyika jana jijini Arusha katika moja ya hotel maarufu ambapo 
viongozi hao walipata wasaa wa kupokelewa na uongozi wa chama cha 
demokrasia na maendeleo (CHADEMA)
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Arusha Onesmo  Ole Nangole  wakati
 akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wananchama wa chadema 
alisema kuwa CCM hivi sasa imekosa misingi iliyounda chama hicho ya haki
 na usawa na kuongeza kuwa hivi sasa kimekuwa ni chama cha watu wachache
 ambao wamekuwa wakichukuaa maamuzi kwa faida yao.
“Nasema
 CCM imekosa misingi iliyounda chama hiki hakuna haki yeyote 
inayotendeka imekuwa chama cha watu Fulani ambao wamekuwa wakichukua 
maamuzi ya kukurupuka kwa faida yao”alisema Nangole
Kwa upande wake  Katibu Mwenezi wa CCM mkoa wa Arusha Isaac Joseph Maarufu kama Kadogoo alisema  kuwa
 kudhirisha kuwa CCM sasa inaendeshwa kwa maslahi ya watu wachache, 
mchakato wa kumpata mgombea Urais wa CCM uligubikwa na mizengwe na 
kusema kuwa kama kanuni na taribu zingefuatwa ni Edward Lowasa ndiye 
angechaguliwa katika mchakato ule.
Pia
 alisema kuwa hawezi kukaa na kuongoza katika chama ambacho wafuasi wake
 wamekihama ,huku akidai kuwa kwa Arusha mjini alikuwa na wafuasi elfu 
ishirini na saba na waliojitokeza kupiga kura ya maoni ya kumpendekeza 
mgombea ubunge kupitia CCM ni elfu tano 
“ Siwezi kubaki kuongoza katika chama  ambacho
 kinabaka demokrasia Uongozi wa CCM watafute viongozi wengine wa 
kuongoza chama hicho siko tayari na siwezi tena”alisema Kadogoo
Mwenyekit
 wa CHADEMA Wilaya ya Arusha Magoma Derick Magoma akiwapokea wanachama 
hao kutoka CCM na kuhamia rasmi CHADEMA anawakaribisha wote wanaoijisika
 kuunga nao na kuleta mabadiliko ya kweli kwa maslahi ya Taifa kwa 
ujumla
“Tunawakaribisha
 wote wanaotaka kuhamia chadema mlango upo wazi mda wowote na siku 
yeyote mda wa mabadiliko ni sasa”alisema Magoma

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni