Mwenyekiti
 wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC),Jaji Mstaafu,Damian Lubuva 
(katikati) akizungumza na waandishi habari juu juu ya maendeleo 
mbalimbali katika kuelekea uchaguzi mkuu uliofanyika leo Makao Makuu ya 
NEC jijini Dar es Salaam,Kulia Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es 
Salaam,Kamishina Suleiman Kova na Kushoto ni Mkuu wa Idara ya Uendeshaji
 Uchaguzi,Clothilde Komba.
 Kamanda
 wa polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam,Kamishina Suleiman Kova 
akizungumza na waandishi habari juu juu  jeshi la polisi lilivyojipanga 
katika suala la ulinzi kuelekea uchaguzi mkuu uliofanyika leo Makao 
Makuu ya NEC jijini Dar es Salaam.
Waandishi
 wa habari wakifatilia wa taarifa ya Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya 
Uchaguzi,Jaji Mstaafu Damian Lubuva leo Makao Makuu ya NEC jijini Dar es
 Salaam. (Picha na Emmanuel Massaka wa Globu ya Jamii) 
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
TUME ya
 Taifa ya Uchaguzi (NEC) inatarajia kuanza kutoa fomu ya urais ,Ubunge 
pamoja na Udiwani kesho na kumalizika kwa zoezi la utoaji fomu hizo ni 
Agasti 21 mwaka huu.
Akizungumza
 na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam,Mwenyekiti wa Tume ya 
Taifa ya Uchaguzi,Jaji Mstaafu,Damian Lubuva  amesema wakati wa 
uchukuaji wa fomu ya urais itatolewa bure lakini wakati wa kurudisha 
anatakiwa kuweka dhamana ya Sh.milioni Moja na wadhamini wadhamini 200 
katika kila mkoa na kuwepo kwa mikoa miwili Zanzibar.
Lubuva
 a amesema kuwa wakati wa kuchukua fomu viongozi wa vyama vya kisiasa 
wanatakiwa kuchukua fomu na kurudisha bila kuwa na kundi kubwa ambalo 
linaweza kusimamisha shughuli za watu wengine.
Amesema
 kwa fomu za ubunge ni sh.50,000  na udiwani sh.5000 ambapo wanatakiwa 
kuchukulia katika ofisi za wilaya na uchukuaji huo lazima uwe wa 
kistaarabu katika kuweza watu wengine waendelee na shughuli zao.
Lubuva amesema kuwa  wanasiasa wanatakiwa  na lugha za kistaarabu katika mikutano yao katika kujenga demokrasia iliyo ya ukweli.
Hata
 hivyo amesema kuna baadhi ya vijana wanauza kadi za tume ya taifa ya 
uchaguzi na kutaka vyombo vya usalama kuchunguza pamoja na kuwachukulia 
hatua watu wanaouza kadi hizo.
Kamanda
 wa Polis wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam,Kamishina Suleiman Kova 
amesema kuwa uchaguzi unaendana  na usalama hivyo jeshi limejipanga 
katika ulinzi katika kipindi hiki.
Kova amesema kuwa Jeshi litaendelea kushirikiana na viongozi wa siasa katika kuleta amani katika kipindi cha uchaguzi.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni