Filamu
 iliyopewa jina la AISHA imezunduliwa rasmi siku ijumaa ya tarehe 
31/7/2015 wilayani Pangani chini ya shirika lisilo la kiserikali la 
UZIKWASA.
Aisha
 ni filamu ya tatu katika mfululizo wa filamu za UZIKWASA zikiangazia 
aina mbali mbali za unyanyasaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto wa 
kike. Filamu hizi ni ni sehemu mojawapo tu ya njia za mawasiliano katika
 kampeni shirikishi-jamii ya mabadiliko ya tabia inayofahamika kama 
'BANJA BASI'!, Pangani, Tanga.
Kabla
 ya filamu ya Aisha iliyozinduliwa kwa kishindo hivi karibuni, shirika 
la UZIKWASA tayari limeshatengeneza filamu nyenigne mbili ambazo ni 
FIMBO YA BABA na CHUKUA PIPI, wengi wa waigizaji waliomo ni wasanii wa 
vijijini.
Pia
 filamu hizi zinatokana na maisha halisi na utafiti wa kina katika 
jamii. Kwa nji hii UZIKWASA inahakikisha filamu zake zinaeleweka na 
zinafanya kazi kama kioo wka jamii. Lengo ni tuone, tuguswe na hatimaye 
tuchukue hatua ili kuleta mabadiliko.
Filamu
 ya AISHA inamhusu mwanamke anayeishi mjini na kuamua kurudi kijijini 
kwao kuhudhuria harusi ya mdogo wake. Wakati anajikumbusha maisha yake 
ya zamani, na kukutana na familia yake pamoja na marafiki, kunatokea 
mkasa wenye athari kubwa katika maisha yake.
Watu wangefumbia macho mkasa huo, lakini Aisha anaamua kupambana nao vikali ili kupata haki yake.
Filamu
 hii inahusu unyanyaa, aibu na wahanga kulaumiwa, na namna gani inazuia 
wanawake na wasichana kusema wazi. Pia inahusu baadhi ya mamlaka na 
viongozi kusita kufatilia ukiukaji wa haki za binadamu.
AISHA
 imeongozwa na mtaalamu maarufu Chande Omar, imetayarishwa kwa 
ushirikiano na Kijiweni Production, imefadhiliwa na A. Schindler na 
Swiss Development Cooperation (SDC) na kusimamiwa na shirika la 
UZIKWASA.
Filamu ya aisha ni kwa heshima ya wanawake wote waliopitia mikasa ya namna hii.
Mkuu wa wilaya ya Pangani Bi Regina Chonjo ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi, nae alipata nafasi ya kutoa hotuba yake.
Producer wa filamu ya Aisha Bwana Emil Shivji akizungumza na wananchi waliohudhuria viwanja vya Bomani.
Mkurugenzi
 wa shirika la UZIKWASA Dokta Vera Piroth akitoa hotuba yake ya kipeke 
ambayo ilikuwa katika mtindo wa hadithi pamoja na maswali, Ilipendeza 
sana.
Shamra
 shamra za ngongoti zikikaribisha wageni waalikwa kwenye uwanja wa 
Bomani wilayani Pangani palipofanyika uzinduzi wa flamu ya Aisha.
Msanii maafuru wa mashairi Ndugu Mabwingo akitoa burudani jukwaani.
Wananchi wakiendelea kufatilia uzinduzi wa filamu ya Aisha.
Msanii mahiri katika uimbaji, Vitalis Maembe alikuwepo kwenye uzinduzi wa filamu ya Aisha, alitoa burudani ya kipekee.
Wasanii waliocheza filamu ya Aisha wakiwa katika picha ya pamoja wakati wakipokea zawadi zao za ushiriki.
Washereheshaji
 katika uzinduzi wa filamu ya Aisha, Mohammed Hammie maarufu kama Anko 
Mo (kati kati), Nickson Lutenda aliyevaa koti la bluu pamoja na Pili 
Mlindwa.
Mkurugenzi wa shirika la UZIKWASA akiteta jambo na mkuu wa wilaya ya Pangani Bi Regina Chonjo.
Msanii
 Godliver Gordian ambaye amecheza kama Aisha katika filamu hiyo, 
akifanya mahojino na kituo cha luninga cha TBC ambao walikuwepo katika 
uzinduzi huo.
Msanii
 Vitalis Maembe akiwa na Godliver Gordian (Aisha), wakati wa utambulisha
 wa wimbo uliotumika kama soundtrack katika filamu hiyo.
Godliver
 Gordian ama Aisha akiwa na mshumaa mara baada ya wananchi kuitazama 
filamu ya AISHA- lengo la mshumaa huo ni kumulika unyanyapaa, pamoja na 
aibu wanayoipata wanawake na wasichana wanapotendewa matendo maovu.
Wageni
 waalikuwa wakiongoza na mkuu wa wilaya Pangani Bi Regina Chonjo nao 
waliwasha mishumaa katika kumuunga mkono Aisha katika harakati za 
kufichua maovu.
Wananchi wengine pia waliwasha mishumaa kuashiria kuunga mkono harakati hizo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni