Mkuu
 wa Masista Waabuduo Damu ya Kristo, Euprasia Julius akimtambulisha 
mgeni rasmi na meza kuu kwa wageni waalikwa na wanakijiji wa Vikawe 
(hawapo pichani) katika hafla ya ufunguzi wa Zahanati ya Da.Ma Africa 
Maria De Mathias (MDM) Vikawe, Kibaha.
Na Mwandishi wetu, Kibaha
MGANGA
 Mkuu wa halmashauri ya Mji Kibaha, Dk. Happniness Ndosi amepongeza 
shirika la masisita wa Waabuduo Damu ya Kristo kwa kufanikisha ujenzi wa
 zahanati ya kisasa katika kijiji cha Vikawe wilayani Kibaha mkoani 
Pwani.
Mganga
 huyo ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla ya uzinduzi wa zahanati 
hiyo,pamoja na kuwapongeza amesema serikali itaendelea kushirikiana na 
mashirika yote kwa lengo la kuwezesha kila kijiji kiwe na zahanati na 
kila kata kituo na kila wilaya kuwa na hospitali.
Aliwapongeza
 masista hao kwa kuonesha upendo na huruma kama Biblia inavyomsimulia 
msamaria mwema ambaye alikuta mtu aliyepigwa na majambazi na kumsaidia.
Mganga
 Mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Kibaha, Dr. Happiness Ndosi akimpa 
mkono wa shukrani Mfadhili aliyejitolea kujenga Zahanati hiyo Raia wa 
Italia, Germano Frioni kwa ujenzi wa Zahanati hiyo itakayohudumia wakazi
 wa kijiji cha Vikawe, Kibaha.
Masista
 Waabuduo Damu ya Kristo wakielekea meza kuu kwa mwendo wa madaha huku 
wakiwa wamebeba zawadi kwa ajili ya kumkabidhi mgeni rasmi na wafadhili 
waliojitolea kujenga Zahanati hiyo.
Aliahidi
 ushirikiano wa serikali katika kufanikisha usajili wa zahanati hiyo na 
kuendelea kuisaidia hatua kwa hatua hadi inakuwa kituo mpaka 
watakapofanikisha safari yao ya kuwa hospitali kubwa ya kisasa.
Mganga
 huyo pamoja na kutoa ahadi hiyo aliwataka wananchi wa Vikawe kutumia 
huduma hiyo na kwamba zahanati hiyo itakapohitaji msaada wa gari la 
kubebea wagonjwa (Ambulance) wataletewa kuchukua mgonjwa na kumfikisha 
panapohusika.
Zahanati hiyo ya DA.MA Africa imejengwa kwa ufadhili wa wakristo wa Italia chini ya usimamizi wa Muitalia, Germano Frioni.
Akitoa
 salamu zake Muitalia huyo amesema kwamba anawashukuru wakazi wa Vikawe 
kwa kumpa nguvu ya kusonga mbele hasa kwa kutambua kwamba yeye na 
marafiki zake wamefanyakazi usiku na mchana kutafuta fedha kwa ajili ya 
kusaidia marafiki wa Afrika.
Alisema atajitahidi kufanya kila linalowezekana kuhakikisha changamoto za zahanati hiyo zinafanyiwa kazi.
Aliwaomba
 wananchi wa Tanzania kuendelea kumuombea yeye na wenzake kama Papa 
Francis anavyoagiza ili malengo ya safari ya kuwapo duniani yafanikiwe.
Alisema
 kwamba watoto wake Daniel na Marco (kwa sasa wote ni marehemu) ambao 
ndio kifupi cha zahanati hiyo DA.MA wamemfanya kujitambua na kusaidia 
wengine katika kuonesha upendo.
Aidha
 alisema kwamba ataendelea kukumbuka Vikawe kwani alifika mara ya kwanza
 mwaka 2005 na kuona hali ilivyokuwa ambapo sasa lipo jengo la zahanati 
hiyo likiwa limekamilika.
Wazo
 la ujenzi wa zahanati hiyo , lilitolewa na wananchi wa Vikawe kwa 
Masisita Waabuduo Damu ya Kristo mwaka 2004 wakati wakiwa katika eneo 
hilo baada ya kununua ekari 40 kwa ajili ya kilimo mwaka 1994.
Alisema
 pamoja na maombi hayo na wao wenyewe kutambua kwamba kuna mahitaji 
makubwa ya huduma ya afya japokuwa kuna zahanati ya serikali, hawakuweza
 kutekeleza maombi ya wanavijiji hadi mwaka 2011 walipofanikiwa kupata 
ufadhili kutoka Italia na kuanza ujenzi mwaka 2013.
Katika
 risala yao walisema kwa ushirikiano kati yao na wafadhili hao 
wamefanikiwa kuwapo kwa zahanati hiyo yenye mahitaji yote ya msingi kwa 
mujibu wa taratibu za serikali na kuzidi.
Msoma risala alisema kwamba wataendelea kupanua miundombinu mpaka zahanati hiyo ifikie ngazi ya cha afya na baadae hospitali.
Pamoja na ujenzi wa zahanati hiyo ya kisasa masisita hao wameanzisha shule ya awali kuwaandaa wanafunzi wa darasa la kwanza.
Wamesema
 kwamba wanaamini kwamba wataendelea kushirikiana na wananchi na wadau 
wengine wa afya katika kuimarisha huduma za hospitali hiyo.
Zahanati
 hiyo pamoja na vifaa tiba pia ina raslimali ya visima vya maji ya mvua 
ujazo zenye ujazo wa lita laki moja na kingine lita 49 elfu, wanatumia 
umeme wa sola na jenereta .
Walisema kwamba wanachangamoto ya kukosa umeme wa Tanesco, barabara nzuri na nyumba za wafanyakazi.
Mwenyekiti wa kijiji cha Vikawe, Kibaha, Shabaan Mgini akiwasalimia wageni waalikwa wakati wa utambulisho.
Sr. Theresia Rogatus akisoma risala katika hafla ya ufunguzi wa Zahanati ya Da.Ma Africa DMD iliyopo Vikawe, Kibaha.
Mganga
 Mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Kibaha, Dr. Happiness Ndosi 
akizungumza kwenye hafla ya ufunguzi wa Zahanati ya Da.Ma Africa -DMD 
kijiji cha Vikawe, Kibaha. Kutoka kushoto ni Mdau wa Zahanati hiyo, Dr. 
Zuberi Mzige wa Hospitali ya Mwananyamala,
Mganga
 Mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Kibaha, Dr. Happiness Ndosi (kulia) 
akimkabidhi zawadi Mfadhili aliyejitolea kujenga Zahanati hiyo Raia wa 
Italia, Germano Frioni. Anaye shuhudia tukio hilo ni Baba Paroko wa 
Parokia ya Bikira Maria wa Mlima Kalmeri Bunju...
Mganga
 Mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Kibaha, Dr. Happiness Ndosi akikabidhi
 zawadi kwa wadau waliombatana na Mfadhili aliyejitolea kujenga Zahanati
 hiyo Muitalia, Germano Frioni.
Mganga
 Mkuu wa halmashauri ya Mji wa Kibaha, Dr. Happniness Ndosi (wa pili 
kulia) pamoja na Mfadhili wa ujenzi wa Zahanati ya Da.Ma Africa ya 
kijiji cha Vikawe, Kibaha, Muitalia, Germano Frioni wakikata utepe 
kuashiria uzinduzi rasmi wa Zahanati hiyo inayosimamiwa na Masista 
Waabuduo Damu ya Kristo nchini.
Muonekano wa ndani ya Zahanati ya Da. Ma Africa-DMD iliyop Vikawe, Kibaha mkoa wa Pwani.
Mganga
 Mkuu wa halmashauri ya Mji wa Kibaha, Dr. Happniness Ndosi akiangalia 
chumba cha dawa katika Zahanati hiyo mara baada ya kuzinduliwa.
Wageni waalikwa wakijadiliana jambo mara baada ya kufungiliwa rasmi Zahanati hiyo nje ya moja ya chumba cha upasuaji mdogo.
Baba
 Paroko wa Parokia ya Bikira Maria wa Mlima Kalmeri Bunju akiendesha 
ibada takatifu ya misa maalum kabla ya ufunguzi rasmi wa Zahanati hiyo.
Wanakijiji wa Vikawe wakishiriki ibada maalum wakati wa uzinduzi wa Zahanati ya Da. Ma Africa.
Kwaya ikitoa burudani.
Wageni waalikwa na wanakijiji wakishiriki kuimba pamoja na kwaya.
Pichani juu na chini ni baadhi ya wanakijiji na wageni waalikwa waliohudhuria uzinduzi huo.
Umati wa wageni waalikwa na wanakijiji wa Vikawe.
Mgeni
 rasmi Mganga Mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Kibaha, Dr. Happiness 
Ndosi katika picha ya pamoja na wadau pamoja na wafadhili waliojenga 
Zahanati hiyo.
Masista Waabuduo Damu ya Kristo wakifurahia taswira za picha za mnato kutoka kwenye kamera.
Jenereta la Zahanati ya Da.Ma Africa linalotumika kutoa umeme katika Zahanati hiyo.
Muonekano wa nje wa jengo la Zahanati ya Da.Ma Africa kabla ya kuzinduliwa rasmi.
Wanakijiji wa Vikawe na wageni waalikwa wakiingia kukagua Zahanati hiyo mara baada ya kuzinduliwa.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni