TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Ofisi
 ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inasikitika 
kuwepo kwa taarifa za uzushi ambazo zimesambaaa kwenye mitandao ya 
kijamii zinazodai kuwa Mheshimiwa Makamu wa Rais  wa Jamhuri ya Muungano
 wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal ataongea na vyombo vya habari 
kuhusu msimamo wake ndani ya Serikali na Chama Cha Mapinduzi.
Habari
 hizi si za kweli na tunaomba kuueleza umma wa Watanzania kuwa 
Mheshimiwa Makamu wa Rais, hausiki na taarifa hizo zilizoenea kwenye 
mitandao ya Kijamii na wala hajapanga tukio lolote la kukutana na 
waandishi wa habari na wala hana mpango wa kuzungumzia msimamo wake 
ndani ya Serikali na Chama Cha Mapinduzi.
Aidha
 tunatumia nafasi hii kuwataka wale wote wenye tabia ya kuvumisha 
taarifa zisizo sahihi kwa maslahi yao waache kufanya hivyo kwa kuwa ni 
kosa kisheria. Tunawaomba waandishi wa habari kufuata taratibu za kazi 
na kutafuta taarifa sahihi kwenye vyombo vinavyohusika na kutambulika.
Boniphace Makene
Mwandishi wa Habari wa Makamu wa Rais

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni