Aliyevalia shati la blue ni Balozi mdogo wa Kenya Tanzania,Boniface Muhia akiondoka katika banda la kampuni ya Simba
 Cement mara baada ya kutembelea banda hilo katika viwanja vya nane nane
 Themi jijini Arusha ,kushoto ni Mkurugenzi wa Kenya plant helth 
inspectorate service Bi.Esther Kimani(Habari Picha na Pamela Mollel wa jamiiblog)
Wananchi
 wakipata elimu katika banda la Simba Cement katika maonyesho ya nane 
nane ya kandaele ya kaskazini yanayoendelea katika viwanja vya njiro 
Themi jijini Arusha
Ugeni kutoka kenya wakiongozwa na Balozi mdogo wa Kenya Tanzania,Boniface Muhia  wakipata maelezo katika banda la Simba Cement 
Afisa masoko Mkuu wa kampuni  ya Simba Cement Leslie Massawe kushoto akitoa maelezo kwa mteja aliyefika katika banda lao katika maonyesho ya nane nane
Tafiti
 zimeonyesha kuwa baadhi ya watumiaji wa saruji hapa nchini hawafati 
viwango vilivyowekwa na hivyo hupelekea kupata bidhaa isiyo bora kwa 
watumiaji wa bidhaa hiyo
Hayo yamebainishwa na afisa masoko Mkuu wa kampuni  ya
 Simba Cement ambao ni watengenezaji wa Saruji  ,Leslie Massawe wakati 
akitoa elimu kwa wananchi waliotembea banda lao katika maonyesho ya nane
 nane ,kanda ya kaskazini  jijini Arusha
Massawe alisema kuwa utafiti uliofanywa na kampuni yao ya saruji inaonyesha kuwa baadhi ya wajenzi hawafuati  mchanganyiko unaokubalika baina ya saruji,mchanga,kokoto hivyo inapelekea kupata matofali yaliyochini ya kiwango 
“Bidhaa
 zetu ni matokeo ya utafiti wa kina na uboreshaji makini unaofanywa na 
wataalumu wetu kupitia ujuzi wao wenye sifa zinazozingatia viwango vya 
ubora wa simenti Tanzania”alisema Massawe
Aidha
 alisema kuwa wanautarabu wa kutoa elimu ya mara kwa mara kwa wateja wao
 pamoja na wananchi kwa ujumla juu ya matumizi sahihi ya saruji ,katika 
ujenzi wa sekta mbalimbali sanjari na uzalishaji wa viwandani hali 
itakayosaidia upatikaniji wa ujenzi wa nyumba imara na miundombinu bora
Alitoa
 wito kwa wananchi kupata elimu ya matumizi bora ya vifaa vinavyotumika 
katika ujenzi kabla ya kuanza ujenzi,huku akiwataka mafundi ujenzi  na watengenezaji wa matofali kutenga muda wa kushiriki semina mbalimbali zinazotolewa na kampuni za saruji

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni