Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikata 
utepe kuashiria ufunguzi wa barabara ya Ndundu - Somanga yenye urefu wa 
kilomita 60, hafla hiyo imefanyika jana Agosti 7 2015 mkoani 
Lindi.Wengine pichani ni Balozi wa Kuwait Jassem Ibrahim Al 
Najem,Mwakilishi wa Mfuko wa Kuwait, Abrahman Al- Hashim,Mkuu wa Mkoa wa
 Pwan, Eng. Evarist Ndikilo, wengine kushoto ni Waziri wa ujenzi 
Mhe.John Pombe Magufuli, Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na Mkuu wa mkoa 
wa Lindi Mhe.Mwantumu Mahiza.
  Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanazia Dkt.Jakaya Kikwete akiwa kwenye picha
 ya pamoja na viongozi mbali mbali mara baada ya kufunguarasmi barabara 
ya Ndundu - Somanga.
 Rais
 Kikwete akimshukuru  Mwakilishi wa Mfuko wa Kuwait ,Abrahman Al Hashim 
mara baada kuweka jiwe la msingi wakati wa sherehe fupi zilizofanyika   
kwenye kijiji cha Marendego ,wakati wa ufunguzi wa barabara ya 
Ndundu-Somanga mkoani Lindi yenye urefu wa kilomita 60 na imejengwa kwa 
kiwango cha lami.
 Rais
 wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete kwa pamoja na mkewe 
Salma  Kikwete akimwagia maji mti wa kumbukumbu alioupanda baada ya 
ufunguzi wa barabara ya Ndundu - Somanga mkoani Lindi.
Wafadhili
 wa ujenzi wa barabara ya Ndundu-Somanga, Balozi wa Kuwait Jassem 
Ibrahim Al Najim na   Mwakilishi wa Mfuko wa Kuwait ,Abrahman Al Hashim 
mara kwa pamoja wakishiriki kupanda mti wakati wa sherehe fupi 
zilizofanyika   kwenye kijiji cha Marendego ,wakati wa ufunguzi wa 
barabara ya Ndundu-Somanga mkoani Lindi yenye urefu wa kilomita 60 na 
imejengwa kwa kiwango cha lami.
 Rais
 Kikwete akiwasalimia na kuwaaga wananchi wa kijij cha Nangurukulu na 
kumtambulisha Mgomea Urais kwa chama cha CCM Dkt John Pombe Magufuli 
alipokuwa akielekea mkoani Lindi.
Mgombea
 Urais wa chama cha Mapinduzi Dkt John Pombe Magufuli akijitambulisha 
kwa wakazi wa mji wa Nangukurulu,mara baada ya sherehe fupi za ufunguzi 
wa barabara ya Ndundu-Somanga kukamilika mkoani Lindi.
 Rais
 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Kikwete akisalimiana na 
Waziri wa Ujenzi ambaye pia ni Mgombea mteule wa Urais wa chama cha 
Mapinduzi,Dkt John Pombe Magufuli alipokuwa akiwasili katika kijiji cha 
Marendengo Wilayani Kilwa mkoani Lindi kufungua barabara ya 
Ndundu-Somanga yenye urefu wa kilometa 6.Barabara hiyo imejengwa na 
Serili ya Tanzania kwa kushirikiana na Ufadhili wa Mfuko wa Kuwait 
pamoja na mfuko wa OPEC .
 Waziri wa Ujenzi Dkt John Pombe Magufuli akipokelewa na  Mkuu
 wa mkoa wa Lindi,Mh.Mwantumu Mahiza mara baada ya kuwasili katika 
kijiji cha Marendengo Wilayani Kilwa mkoani Lindi kushiriki ufunguzi wa 
barabara ya Ndundu-Somanga yenye urefu wa kilometa 6.Barabara hiyo 
imejengwa na Serili ya Tanzania kwa kushirikiana na Ufadhili wa Mfuko wa
 Kuwait pamoja na mfuko wa OPEC .

 Waziri
 wa Ujenzi Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri wa Mambo ya 
Nje na ushirikiano wa Kimataifa,Mh.Bernad Membe mara baada ya kuwasilia 
katika kijiji hicho  Marendengo,ambapo
 sherehe za uzinduzi wa barabara ya Ndundu-Somanga zilifanyika na mgeni 
Rasmi alikuwa ni Rais Dkt Jakaya Kikwete.
 Dkt
 John Pombe Magufuli akisalimiana na Mke wa Rais Mama Salma 
Kikwete,kushoto kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam,Mh Said Meck 
Sadick akiwa sambama na Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mh.Mwantumu Mahiza.
Wananchi
 kutoka kijiji cha Marendego na vijiji vyake wakishangilia jambo wakati 
wa ufunguzi wa barabara ya Ndundu –Somanga yenye urefu wa kilometa 
6,inayojengwa na Tanzania kwa kushirikiana na Ufadhili wa mfuk wa Kuwait
 pamoja na Opec.Katika unziduzi huo viongozi mbalimbali wa chama na 
serikal,viongozi wa dini pamoja na watu wengine walishiriki kushuhudia 
tukio hilo adhimu hapa nchini.
 Wananchi wakifuatilia tukio hilo
 Dkt
 John Pombe Magufuli akisalimiana na viongozi mbalimbali wa chama na 
serikali wakati wa ufunguzi wa barabara hiyo ya Ndundu -Somanga yenye 
urefu wa kilometa 60
 Wananchi wakifurahia ufunguzi wa barabara hiyo iliyokuwa kero kubwa kwa wananchi wa Mtwara na Lindi
  Waziri
 wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe 
akizungumza na Waziri wa Ujenzi Dk.John Pombe Magufuli wakati wa sherehe
 fupi za ufunguzi wa barabara ya Ndundu-Somanga iliyojengwa kwa kiwango 
cha lami na yenye urefu wa kilometa 60 ,Somanga mkoani Lindi.
 Rais Kikwete akisalimiana na Waziri wa Mambo ya nje na ushirikiano wa Kimataifa,Mh Bernad Membe
  Rais
 Jakaya Mrisho Kikwete akiwasalimu wananchi waliojitokeza kushuhudia 
ufunguzi wa barabara ya Ndundu - Somanga yenye urefu wa Kilomita 60 
mkoani Lindi.
  Rais
 Jakaya Mrisho Kikwete akiwasalimu wananchi waliojitokeza kushuhudia 
ufunguzi wa barabara ya Ndundu - Somanga yenye urefu wa Kilomita 60 
mkoani Lindi.
  Rais
 Jakaya Mrisho Kikwete akiwasalimu wananchi waliojitokeza kushuhudia 
ufunguzi wa barabara ya Ndundu - Somanga yenye urefu wa Kilomita 60 
mkoani Lindi.
 Waziri
 wa Ujenzi Dk.John Pombe Magufuli akihutubia wananchi wakati wa sherehe 
fupi zilizofanyika   kwenye kijiji cha Marendego kata ya Somanga za 
ufunguzi wa barabara ya Ndundu-Somanga mkoani Lindi yenye urefu wa 
kilomita 60 na imejengwa kwa kiwango cha lami.
  Rais
 wa Jamhuri ya Muungano Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wananchi 
wakati wa sherehe fupi ya ufunguzi wa barabara ya Ndundu-Somanga mkoani 
Lindi yenye urefu wa kilomita 60 na imejengwa kwa kiwango cha lami.





















Hakuna maoni:
Chapisha Maoni