Mkurugenzi
 Mkuu wa Shirika la NYUMBU (Tanzania Automative Technology Centre) 
Brigedia Jenerali Anselim akiongea na waandishi wa Habari (hawapo 
pichani) kuhusu miradi mbalimbali iliyotekelezwa na shirika hilo 
inayodhamiria kuwawezesha wananchi kiuchumi ikiwemo utengenezaji wa 
matrekta madogo( power Tiller) ambayo yanalenga kumkomboa mkulima hapa 
nchini kwa kuondokana na matumizi ya jembe la makono.
 Baadhi
 ya waandishi wa habari wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la 
NYUMBU (Tanzania Automative Technology Centre) Brigedia Jenerali 
Anselim.
 Mkuu
 wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la 
Kujenga Taifa Luteni Kanali Juma Nkangaa Sipe akiongea na Waandishi wa 
Habari (hawapo pichani) umuhimu wa kutoa habari za kuelimisha kwa jamii 
hasa zitakazowawezesha kuwajengea uwezo wa kimaarifa na kuwainua kichumi
 kupitia elimu hiyo.
Mhandisi
 Mkuu Msanifu Albert Wikedzi akiwaonesha waandishi wa Habari (Hawapo 
pichani) aina mbalimbali za sanifu zinazofanyika katika shirika hilo, 
wakati wa ziara ya waandishi wa habari katika kiwanda hicho Mjini  kibaha.
 .Mhandisi
 Mkuu wa Karakana kutoka Shirika la NYUMBU (Tanzania Automative 
Technology Centre) Ayoub Mnzava akiwaonesha waandishi wa habari trekta 
ndogo (Power Tiller) iliyotengenezwa kwa lengo la kuongeza uwezo wa 
wazalishaji wa mazao ya kilimo kote nchini.
 Mkuu
 wa Kitengo cha Usubiaji Mhandisi Anderson Ole Zakaria akiwaeleza 
waandishi wa habari namna kitengo hicho kinavyofanya kazi ili kukidhi 
mahitaji ya kiwanda ambapo alisema kitengo hicho kinayeyusha hadi tani 
2.5 za chuma zinazotumika kutengeneza bidhaa mbalimbali zinazotoka 
katika shirika hilo.
 Mkurugenzi
 Mkuu wa Shirika la NYUMBU (Tanzania Automative Technology Centre) 
Brigedia Jenerali Anselim akiwaonesha waandishi wa habari moja aina ya 
gari la kivita lililotengezezwa na shirika hilo.
.Mkurugenzi
 Mkuu wa Shirika la NYUMBU (Tanzania Automative Technology Centre) 
Brigedia Jenerali Anselim (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na 
waandishi wa habari waliokuwa katika ziara hiyo,kulia ni Mkuu wa Kitengo
 cha Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga 
Taifa Luteni Kanali Juma Nkangaa Sipe na kushoto ni mwandishi mwandamizi
 wa Channel Ten.
PICHA NA HASSAN SILAYO-MAELEZO






Hakuna maoni:
Chapisha Maoni