Mkuu wa Wilaya ya 
Arumeru mkoani Arusha, Mh. Jerry Muro amefungua mkutano wa wabobezi wa 
utafiti katika ukanda wa Africa Mashariki ” The Eastern Africa Research 
and Innovation Management Association, Tanzania Chapter, mapema hii leo.
Dc Muro 
amemuwakilisha Mkuu wa mkoa wa Arusha. Mh. Mrisho Mashaka Gambo Mkuu wa 
Wilaya amewapongeza Watafiti kwa Ubunifu wa kuwa na Jukwaa la Pamoja 
kutafuta suluhisho la changamoto zinazowakabiri wananchi wa jumuia ya 
Africa ya Mashariki.
Pia amewaeleza juhudi
 mbali mbali ambazo zinafanywa na Serikali yaTanzania za kuwezesha 
taasisi za kitafiti na za Elimu ya juu katika utafiti.
Ameeleza kuwa 
serikali inasubiria kupata mrejesho juu ya changamoto mbali mbali 
zitakazo bainishwa na wataalam hao ili kuendelea kutoa ushirikiano 
stahiki katika kuzifanyia kazi changamoto hizo Dc Jerry Muro, 
ameipongeza Taasisi ya Sayansi na Technolojia ya Nelson Mandela, iliyoko
 Tengeru, Arusha kwa kuonesha mfano mzuri wa tafiti zinazogusa maisha ya
 watu na viwanda na kusema kuwa kazi kubwa iliyobakia ni kushirikiana 
katika kuzifikisha kwa jamii na viwanda.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni