Mkurugenzi wa fedha na mpango katika hospitali ya Rufaa Bugando, mtawa Suzan Bathlomeo amefariki dunia baada ya kujirusha kutoka gorofani muda mfupi baada ya kutoka kusali misa ya saa 12:00 asubuhi, leo Jumanne Agosti 28, 2018.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Jonathan Shana 
amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa taarifa kamili 
atazungumza na waandishi wa habari baadaye.
Kwamjibu wa ofisa uhusiano wa Bugando, Lucy Mogele amesema 
mtawa huyo amefariki dunia leo alfajiri, huku akibainisha kuwa hospitali
 hiyo haina mamlaka ya kuzungumziwa suala hilo na kutaka litafutwe 
shirika la watawa la Kagera, ambalo makao makuu yake yapo mjini Bukoba 
mkoani Kagera.
 “Ni kweli Sister Suzan amefariki dunia baada ya kujirusha 
kutoka ghorofani lakini Bugando hatuna mamlaka ya kuzungumzia suala 
hilo,” amesema Lucy.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni