Na Ahmed Mahmoud
Serikali imeahidi kuendelea kuziwezesha kifedha taasisi 
 mbalimbali zinazojihusisha na  utafiti vikiwemo vyuo vikuu ili kuleta 
tija kwa taifa kufikia uchumi wa kati 
Akifungua Mkutano wa nne wa jumuia ya watafiti kutoka nchi 
za Afrika Mashariki (EARIMA), unaofanyika jijini Arusha,Mkuu wa wilaya 
ya Arumeru ,Jerry Muro akimwakilisha mkuu wa mkoa wa Arusha,amesema kuwa
 serikali itaendelea  kugharamia tafiti hizo ili kuwawezesha kuwafikia 
wakulima na wafugaji waweze kukua kiuchumi.
Amewaomba watafiti hao kuelekeza nguvu zao katika tafiti 
zinazofikika kwa jamii katika ukanda wa Afrika Mashariki kuhakikisha 
tafiti zao zinalinufaisha taifa na wananchi wake katika kushiriki 
shughuli za maendeleo
"Wataalamu na wabobezi wa tafiti mbalimbali mtusaidie 
kuzifanya tafiti hizi kuleta tija ili kulifikisha taifa katika uchumi wa
 kati"Amesema Muro
Amewataka watafiti hao kutoka nchi za Afrika Mashariki 
kuunganisha nguvu ya kutafuta njia zitakazosaidia tafiti zinazofanyika 
katika nchi hizo ziweze kwenda kwenye utekelezaji, hususani zile 
zinazolenga kutatua changamoto zinazowakabili wananchi wa Mataifa hayo.
Naye Mwenyekiti wa jumuiya ya watafiti wa Nchi za Afrika Mashariki (EARIMA), upande wa Tanzania Dk. Alfred Sebahene, amesema mkutano huo umekuja baada ya kuwa tafiti nyingi zinazofanywa bado hazijaleta tija ya kuchangia uchumi wa nchi hizo hususani katika kutatua matatizo yaliyopo kwenye sekta za kilimo na Mifugo.
Amesema mkutano huo utajadili na kutoka 
na mapendekezo yatakayosaidia tafiti zinazofanywa ziweze kwenda kutatua 
changamoto zinazoikabili jamii ya mataifa hayo.
Amesema tafiti nyingi katika nchi 
mbalimbali za Afrika Mashariki zinafanana ila changamoto kubwa ni 
kutokana na mazingira yaliopo na hivyo mkutano huo utasaidia 
kubadilishana uzoefu .
Kwa upande wake mkuu wa sekretarieti ya 
EARIMA ambaye ni mhadhiri mwandamizi wa chuo kikuu cha Dar es salaam Dk.
 Edwinus  Lyaya amesema watafiti wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya 
bajeti ya kufikisha tafiti zao kwa jamii.
Amesema mkutano huo unalenga kusimamia 
utafiti na ugunduzi na kuhimiza tafiti za wataalamu ziweze kutoka kwenye
 makablasha na kuwafikia wananchi.
"Tunajadiliana ili kuzitoa tafiti kwenye 
maandishi na kufikia kwenye vitendo ili tafiti hizo ziweze kuzaa matunda
 kwa jamii" Amesema
Mmoja wa Watafiti kutoka Chuo kikuu cha 
Nelson Mandela Prof.Charlea Lugomela  alisema  chuo chao kimeshaanza 
kutoa tafiti mbalimbali zenye matumaini kwa Wakulima na Wafugaji.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni