MBUNGE wa Mtwara Vijijini (CCM) 
ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Bajeti, Hawa Ghasia na 
Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Jitu Soni wamejiuzulu nafasi hizo, leo
 Jumanne Agosti 28, 2018.
Ghasia na Soni ambaye pia ni 
Mbunge wa Babati Vijijini wametangaza uamuzi wao leo asubuhi mbele ya 
wajumbe wa kamati hiyo jijini Dodoma.
Bado haijafahamika sababu za viongozi hao kufanya uamuzi ho wa kujiuzulu.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni