Rais Trump atishia kuichukulia hatua mitandao ya Google, Twitter na Facebook kwa kupotosha taarifa zake

Rais wa Marekani Donald Trump amezionya kampuni za mawasiliano ya mtandao Google, Twitter na Facebook na kusema kuwa ataichukulia hatua kutokana na  kile alichokiita kuminya taarifa zake na za mrengo wa kihafidhina.
Licha ya Rais Trump hajabainisha ni hatua gani hasa ambazo utawala wake unapanga kuzichukua.
Trump ameitaka mitandao hiyo kuwa makini baada ya awali kuishutumu Google kwa kupindua matokeo ya taarifa pale mtumiaji wa mtandao huo anapotafuta habari kumhusu Trump.
Hata hivyo, Google wamekanusha shutuma kuwa mtandao wao unaupendeleo na kusema hawafungamani na itikadi yoyote ya kisiasa.
Chanzo:BBC Swahili.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni