Snura Mushi
Msemaji wa Msanii Snura Baraka Nyagenda. akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salamm leo.
Msanii Snura Mushi (kulia), akizungumza
katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, kuhusu
Serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imeruhusu
kupigwa kwa wimbo wa chura ya kuufunga kwa kuwa haukuwa na maudhui
mazuri ya kitanzania. Kushoto ni Msemaji wake, Baraka Nyagenda.
Mkutano na wanahabari ukiendelea.
N a Dotto Mwaibale
SERIKALI kupitia Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo imeruhusu kupigwa kwa wimbo wa chura wa
msanii Snura Mushi baada ya kuufunga kwa kuwa haukuwa na maudhui mazuri
ya kitanzania.
Akizungumza katika mkutano na waandishi
wa habari Dar es Salaam leo, Snura Mushi alisema wimbo wake na video
umeruhusiwa kupigwa baada ya audio ya chura kufanyiwa marekebisho na
kuifanya kuwa katika maudhui ya kitanzania.
Alisema ruhusa hiyo imetolewa kwa barua
iliyoaandikiwa Septemba 26, 2016 yenye kumbukumbu HA.26/375/01'B'/137
ambayo gazeti hili lina nakala yake.
Kupitia mkutano huo msanii Snura Mushi
kwa mara nyingine aliomba radhi kwa watanzania na Serikali kwa ujumla
kwa usumbufu walioupata kwa video yake ya kwanza na kuwaomba waendelee
kuiona video mpya iliyorekebishwa baada ya kuifuta ya kwanza.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni