Na Mwamvua Mwinyi,Kibaha
NAIBU 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI,Selemani Jafo,amesema mkoa wa 
Pwani umepokea Bil.2.340 zitakazotumika kugawanywa kwenye vituo vya afya
 na zahanati 234 zilizopo mkoani hapo ili kuboresha na kutatua 
changamoto zilizopo.
Amesema
 fedha hizo zimetolewa kutoka katika mpango wa malipo kwa ufanisi 
unaotekelezwa kwa ushirikiano baina ya bank ya dunia na serikali ya 
Tanzania kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.Aidha Jafo amewasihi 
wakurugenzi,wenyeviti wa halmashauri na mganga mkuu wa mkoa 
huo,kusimamia fedha hizo ili ziweze kuleta tija .
Katika
 hatua nyingine,ametoa wiki moja hadi kufikia februari 21 mwaka huu,kwa 
waganga wakuu wa mikoa (RMO)na makatibu tawala wa mikoa (RAS)kote 
nchini,kuhakikisha wanapeleka account za bank zinazotumiwa katika vituo 
na zahanati zote.Alhaj Jafo,aliyasema hayo wakati akizungumza na 
wakurugenzi na wenyeviti wa halmashauri pamoja na waganga wakuu wa 
wilaya mkoani Pwani.
Alisema
 kati fedha hizo kila zahanati na kituo cha afya kitapatiwa kiasi cha 
sh.mil 10 ili kuboresha na kutatua kero sugu zilizokuwa 
zikiwasumbua.“Kuna zahanati na vituo vya afya ambavyo havina 
magodoro,mapaa yamebomoka,,hakuna vyoo huku nyumba za mganga wa kituo 
nayo ikiwa haina choo”“Kuna maeneo mengine hayana hata vitanda vya 
kujifungulia,akinamama wanapata shida yaani unahofia wanaweza kuondoka 
hata na magonjwa mengine,hivyo kwa mazingira haya fedha hizi endapo 
zitatumika kikamilifu zitaondoa matatizo hayo”alisema Jafo.
Alisema
 katika miaka iliyopita fedha hizo zilikuwa hakuna hivyo kutokana na 
mpango huo kuanza,wahakikishe wanaleta matokeo chanya kwa kujibu 
changamoto zilizokuwa zikiwakabili.Jafo alisema hatofurahishwa akisikia 
mradi huo haujafanikiwa katika mkoa wa Pwani na mikoa mingine 8 ambayo 
ipo kwenye mradi huo kwa majaribio hapa nchini.
Akizungumzia
 suala la utoaji huduma bora za kiafya,alieleza kuwa ni tatizo kubwa na 
aibu kwani katika mkoa huo jumla ya vituo 153 vina nyota 0(0 star)kati 
ya vituo 234 vilivyopo .Alifafanua kuwa vituo vinavyokosa star kubwa 
ndivyo vinavyokosa mapato zaidi kwani endapo hospitali inafanya vizuri 
inapata mil.360,kituo cha afya mil.79.8 na zahanati mil.19.
“Hili 
ni tatizo la nchi nzima,niwaombe waganga wakuu wa wilaya na mikoa 
kusimama kidete,kuhakikisha mnaondoa hizi 0,sifuri hizi hazina maana 
,zinashusha mapato,kuanzia sasa mfanye juhudi mpate nyota 4 hadi 
5”alisema Jafo.Alimtaka mganga mkuu wa mkoa wa Pwani,dk Beatrice 
Byarugaba,kuacha kukaa ofisini badala yake atoke kutembelea vituo na 
zahanati mbalimbali ili kujiridhisha na huduma inayotolewa.
Wakati
 huo huo, Jafo alitoa wiki moja kwa makatibu tawala wa mikoa na waganga 
wakuu nchini kupokea account zote za vituo na zahanati zilizopo kwenye 
mikoa yao .Waziri huyo alisema endapo mkoa wowote utashindwa kutekeleza 
agizo hilo basi katibu tawala na mganga mkuu wa mkoa husika watatakiwa 
kutoa maelezo.
Nae 
mchumi idara ya afya kutoka TAMISEMI,Nassoro Shemzigwa,alisema mpango 
huo unatekelezwa katika mikoa tisa ikiwemo 
Pwani,Shinyanga,Mwanza,Simiyu,Geita,Kagera na Mara .Alielezea kuwa lengo
 la mradi ni kuboresha huduma za afya ya msingi kuanzia hospital ya 
wilaya,zahanati na vituo vya afya.Shemzigwa alisema mpango huo 
utatekelezwa kwa kipindi cha miaka mitano kuanzia mwaka 2015/2016 hadi 
2020 na utakuwa ni endelevu.
Mwenyekiti
 wa halmashauri ya wilaya ya Kibiti,Khatibu Chaurembo,alibainisha 
wamepokea maagizo na maelekezo waliyopewa na wataenda kuyafanyia 
kazi.Chaurembo aliiomba serikali kuangalia tatizo la uhaba wa watumishi 
katika zahanati mbalimbali hasa maeneo ya vijijini ambako zipo zahanati 
zenye mtumishi mmoja hivyo kusababisha huduma kuzorota.
NAIBU 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI,Selemani Jafo,akizungumzia na 
wakurugenzi,wenyeviti wa halmashauri,waganga wakuu wa wilaya mkoani 
Pwani,jana.(Picha na Mwamvua Mwinyi) 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni