Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji ,Charles Mwijage
 amewataka watanzania kuwekeza katika mfumo unaoweza kutoa ajira za moja
 kwa moja kwa vijana kama ilivyo katika kampuni ya Manjano Foundation.
Mwijage
 amesema hayo mapema leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akifungua 
mafunzo ya wanafunzi 30 juu ya masuala ya urembo yanayoendeshwa ta 
tasisi ya Manjano Foundation ya hapa hapa nchini.
“huyu
 ni moja ya wawekezaji ambao wanapaswa kuungwa mkono na kila mmoja kwani
 ameamua kuwekeza kwa kutengeneza bidhaa ambazo zinatumia malighafi 
kutoka hapa hapa nchini na kuamua kuwawezesha wanawake wadogo kupata 
mafunzo hili waweze kuingiza pesa kupitia bidhaa hizo” amesema Waziri 
Mwijage.
Mwijage
 ameongeza kuwa mbali na Manjano foundation kutoa elimu ya ujasiliamali 
kwa wasichana hao pia ipo katika mpango kabambe wa kujenga kiwanda mjini
 kibaha ambapo tayari wameshapata ekeri tatu kwa ajili yakujenga Godown 
ambalo litasaidia kufanya uzalishaji.
Kwa
 upande wake mkurugenzi wa Manjano Foundation Shekha Nasser amesema kuwa
 wasichana ambao wanapata mafunzo kutoka tasisi hiyo wanaweza kuingiza 
kiasi cha Milioni mbili mpaka tatu kwa mwezi.
Aidha
 ametaja kuwa program hiyo katika mwaka hu itaweza kuwafikia wanawake 
katika mikoa mitano nchini hili waweze kujikwamua kiuchumi.
Waziri
 wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage  akipokelewa na 
Mwasisi wa Taasisi ya Manjano na Mmiliki wa Shear Illusions, Shekha 
Nasser mara baada ya kuwasili kwa ajili ya ufunguzi wa mafunzo kwa 
wanawake ikiwa ni awamu ya pili.
Waziri
 wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage akipata maelezo 
kutoka kwa Mwasisi wa Taasisi ya Manjano na Mmiliki wa Shear Illusions, 
Shekha Nasser  kuhusu darasa linalotumika katika ufundishaji wa 
wasichana hao leo katika ofisi ya Shear Illusion iliyopo jengo la 
Millenium Tower jijini Dar
Waziri
 wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage akizungumza na 
wanafunzi wa Manjano Academic mara baada ya kufika na kujionea mafunzo 
hayo leo katika ofisi ya Shear Illusion jijini Dar
Waziri
 wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage akizungumza 
wakati wa uzinduzi wa programu ya kuwawezesha wanawake kiuchumi 
ijulikanayo kama "Manjano Dream Makers" kwa awamu ya pili iliyozinduliwa
 leo na waziri huyo katika ukumbi wa LAPF Millenium Towers jijini Dar es
 Salaam leo.
Mwasisi
 wa Taasisi ya Manjano na Mmiliki wa Shear Illusions, Shekha Nasser 
akizungumza kuhusu uzinduzi rasmi wa program ya ajira kupitia tasnia 
ndogo ya urembo pamoja na kufanya utambulisho kwa wageni waalikwa.
Afisa
 Kutoka TFDA Bi. Grace Shimwela akizungumzia umuhimu wa kupata vibali 
vya urembo "Cosmetics and Personal Care" kwa wanawake walioko na ambao 
wamemaliza progamu mbalimbali za mafunzo kutoka kwa Manjano Dream Maker 
ili kuwasaidia pale wanapoanza kujitegemea
Jokate Mwegelo akizungumza jambo kwenye ufunguzi huo
Mshiriki
 mmoja aliyenufaika na Taasisi ya Manjano, Josephine Rwetela 
akizungumzia umuhimu wa kutengeneza ajira kupitia Tasnia ndogo ya Urembo
 nchini.
Mkurugenzi
 wa GS1 Tanzania, Fatma Khange akitoa maneno ya shukrani kwa wageni 
waalikwa pamoja na wanawake wanaoshiri kwenye mafunzo hayo 
yaliyoziduliwa leo na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. 
Charles Mwijage.
Baadhi ya washiriki walioudhuria katika uzinduzi huo
Waziri
 wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage akimkabidhi 
cheti Mkurugenzi Mtendaji 8020 Fashion na Mentor wa Taasisi ya Manjano 
Foundation, Shamim Mwasha
Waziri
 wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage akimkabidhi cheni
 Mentor wa Taasisi ya Manjano Foundation, Mboni Masimba
Waziri
 wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage  akimkabidhi 
cheti Mentor wa Taasisi ya Manjano Foundation, Mariam Marion Ndaba
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage  akiwa kwenye picha ya pamoja na Manjano Academic
Mgeni
 rasmi Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage 
akiwa kwenye picha ya pamoja na Mentor wa Taasisi ya Manjano Foundation.
Mgeni rasmi Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage akiwa kwenye picha ya pamoja na Dream Makers.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni