Waziri
 wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mh. Nape Nnauye (wa pili kulia)
 akimpongeza Meneja wa Redio Jamii Orkonerei  FM, Baraka David Ole Maika
 baada ya kuwasilisha risala ya mafunzo ya ufundi kwa Redio za Jamii 
wakati maadhimisho ya siku ya Redio Duniani yaliyofanyika katika ukumbi 
wa mikutano wa Chuo Kikuu Huria jijini Dar es Salaam jana. Kulia  
Mkurugenzi wa Utangazaji wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), 
Fredrick Ntobi, Wa tatu kulia ni Mkuu wa Ofisi na Mwakilishili wa 
Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na 
Utamaduni (UNESCO), Zulmira Rodrigues, Wanne kulia Mkurugenzi wa Taasisi
 ya Elimu na Menejementi ya Teknolojia  wa Chuo Kikuu Huria (OUT), Dr. 
Edephonce Nfuka na Wa kwanza kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Mtandao wa 
Vyombo vya Habari vya Jamii (COMNETA), Prosper Kwigize.
 Mgeni
 rasmi Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Nape Nnauye 
akizungumza kwenye sherehe za maadhimisho ya siku ya redio duniani 
yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo Kikuu Huria (OUT) jijini
 Dar es Salaam.
  Afisa
 Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Stella Vuzo 
akisheheresha kwenye sherehe za maadhimisho ya siku ya radio duniani 
yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo Kikuu Huria (OUT) jijini
 Dar es Salaam
 Mkuu
 wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia
 Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini Zulmira Rodrigues akitoa 
neno la ukaribisho liliombatana na ujumbe maalum kwenye sherehe za 
maadhimisho ya siku ya redio duniani yaliyofanyika katika ukumbi wa 
mikutano wa Chuo Kikuu Huria (OUT) jijini Dar es Salaam.
 Makamu
 Mwenyekiti wa Mtandao wa Vyombo vya Habari vya Jamii (COMNETA), Prosper
 Kwigize akisoma hotuba mbele ya mgeni rasmi Waziri Nape Nnauye (hayupo 
pichani) wakati wa sherehe za maadhimisho ya siku ya redio duniani, 
yaliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Chuo Kikuu Huria (OUT) jijini
 Dar es Salaam.
 Mgeni
 rasmi Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Nape Nnauye 
akiteta jambo na Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa 
Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini 
Zulmira Rodrigues (katikati) wakati wa sherehe za maadhimisho ya siku ya
 redio duniani yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo Kikuu 
Huria (OUT) jijini Dar es Salaam. Kushoto ni  Mkurugenzi wa Taasisi ya 
Elimu na Menejementi ya Teknolojia  wa Chuo Kikuu Huria (OUT), Dr. 
Edephonce Nfuka
 Mgeni
 rasmi Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Nape Nnauye 
akimpongeza Makamu mwenyekiti wa Umoja wa Redio za Jamii (COMNETA) 
Prosper Kwigize kwa hotuba nzuri wakati wa sherehe za maadhimisho ya 
siku ya redio duniani yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo 
Kikuu Huria (OUT) jijini Dar es Salaam. Kushoto ni  Mkurugenzi wa 
Taasisi ya Elimu na Menejementi ya Teknolojia  wa Chuo Kikuu Huria 
(OUT), Dr. Edephonce Nfuka na kulia ni Mkurugenzi wa Utangazaji wa 
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Fredrick Ntobi.
 Mkurugenzi
 wa Utangazaji wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Fredrick Ntobi
 akizungumza kuhusu taratibu na sheria za utoaji leseni kwa redio za 
jamii nchini wakati wa sherehe za maadhimisho ya siku ya redio duniani 
yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo Kikuu Huria (OUT) jijini
 Dar es Salaam.
  Mkurugenzi
 wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Dk. Ayoub Rioba akifafanua 
jambo wakati wa sherehe za maadhimisho ya siku ya redio duniani 
yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo Kikuu Huria (OUT) jijini
 Dar es Salaam.
 Meneja
 wa Redio Jamii Orkonerei  FM, Baraka David Ole Maika akitoa neno la 
shukrani wakati wa sherehe za maadhimisho ya siku ya redio duniani 
yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo Kikuu Huria (OUT) jijini
 Dar es Salaam.
 Washiriki
 kutoka redio za jamii nchini na waandishi wa habari waliohudhuria 
sherehe za maadhimisho ya siku ya redio duniani yaliyofanyika katika 
ukumbi wa Cho Kikuu Huria (OUT) jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi
 wa Utangazaji wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Fredrick Ntobi
 akiwasilisha mada kuhusu upashanaji wa vyombo vya habari na sheria 
wakati wa sherehe za maadhimisho ya siku ya redio duniani yaliyoratibiwa
 na UNESCO na kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo Kikuu Huria 
(OUT) jijini Dar es Salaam.
  Mshauri
 wa Masuala ya Uchumi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP)
 Tanzania, Rogers Dhliwayo akizungumza kuhusu malengo ya maendeleo 
endelevu (SDGs) na namna radio inavyowezesha hamasa ya utekelezaji wake 
kwenye sherehe za maadhimisho ya siku ya redio duniani yaliyoratibiwa na
 UNESCO na kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo Kikuu Huria (OUT)
 jijini Dar es Salaam.
Meza
 kuu kwenye sherehe za maadhimisho ya siku ya redio duniani 
zilizofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo Kikuu Huria (OUT) jijini
 Dar es Salaam.
 Mgeni
 rasmi Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Nape Nnauye 
(katikati) katika picha ya pamoja na wawakilishi wa redio za jamii 
nchini wakati sherehe za maadhimisho ya siku ya redio duniani 
yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo Kikuu Huria (OUT) jijini
 Dar es Salaam.
 Mgeni
 rasmi Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Nape 
Nnauye(katikati) na meza kuu katika picha ya pamoja na wajumbe wa bodi 
ya COMNETA wakati wa sherehe za maadhimisho ya siku ya redio duniani 
yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo Kikuu Huria (OUT) jijini
 Dar es Salaam.
  Mgeni
 rasmi Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. Nape 
Nnauye(katikati) na meza kuu katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa 
Umoja wa Mataifa kwenye sherehe za maadhimisho ya siku ya redio duniani 
yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo Kikuu Huria (OUT) jijini
 Dar es Salaam.
Maafisa
 wa UNESCO Dar Luiana Temba (kushoto) na Rose Mwalongo Mataifa 
wakifurahi jambo kwenye sherehe za maadhimisho ya siku ya redio duniani 
yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo Kikuu Huria (OUT) jijini
 Dar es Salaam.
Na Mwandishi wetu
SERIKALI
 imewataka wanahabari kusoma sheria, taratibu na kanuni zinaogusa tasnia
 yao ili iweze kuendelea na kuachana na kuamini kila kitu wanachoambiwa 
na mtu mmoja.
Kauli
 hiyo imetolewa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh. 
Nape Nnauye wakati  akizungumza katika siku ya radio duniani, hafla 
iliyofanyika Chuo Kikuu Huria jijini Dar es Salaam.
"Watu
 someni sheria, taratibu na kanuni kwa kina ili kujua na kuzielewa, 
mkielewa kama kuna sheria inakwaza ukuaji wa sekta ya habari tuseme 
tukae chini.. " alisema Waziri Nape akijibu hoja kuhusu sheria za habari
 zilizopo ambazo zinadaiwa kukwaza uhuru wa ukusanyaji wa habari.
Ilielezwa
 katika hafla hiyo kuwa sheria za sasa ya takwimu na habari  zinakwaza 
uhuru wa sekta hiyo muhimu kwa maendeleo ya taifa.
Katika
 hoja hiyo Makamu mwenyekiti wa Umoja wa Redio za Jamii (COMNETA) 
Prosper Kwigize katika hotuba yake kwa Serikali, alisema kwamba redio 
hizo zinachangamoto nyingi katika utendaji wake ikiwamo sheria 
zilizopo,watoa habari wasioeleweka na wanazuia upatikanaji wa habari.
Nape
 alisema kwamba sheria si msaafu na kwa kuwa asilimia 80 za habari 
zinazalishwa na serikali, waandishi wanahaki ya kupata habari hizo na 
kama kuna kikwazo ni lazima kitafutiwe suluhu.
"Tukae
 tushindane kwa hoja tukubaliane na kuhakikisha kwamba tunarekebisha.. 
Bunge kazi yake ni kutunga na kufuta sheria" alisema Nape ambaye alisema
 kwamba sheria ya sasa imetoa nguvu kwa watoa habari na kwamba si kila 
habari iliyopo serikalini ni classified.
Alisema
 pia ili kufanikisha upatikanaji wa habari maofisa habari wamepewa 
maagizo ya kushiriki vikao ili waweze kutoa taarifa bila woga na kwa 
ujasiri mkubwa.
Alisema
 ni kazi ya serikali ni kutengeneza mazingira mazuri ya kukua kwa tasnia
 ya habari na itaendelea kupigania hilo kwa kuwa inatambua umuhimu wa 
vyombo vya habari.
Pamoja
 na kuweka mazingira mazuri amewataka wanaoendesha redio za jamii 
kutafuta namna ya kujiunga na taarifa za kitaifa (habari) ili wananchi 
wasitengwe na matukio ya maeneo mengine.
Alisema kwa kuwa sehemu kubwa ya redio hizo ziko pembezoni ni vyema nguvu yake ikatumika pia kuhabarisha matukio ya kitaifa.
Akizungumzia
 dawa za kulevya, Waziri Nape alitaka wanahabari kuwa na uzalendo na 
kushiriki katika vita hiyo kwa kutumia vyombo vyao vyote.
Alisema
 ni vyema wananchi na wanahabari wakatambua kwamba vita hiyo ni yetu 
sote na kwamba wanahabari wanauwezo wa kuunganisha wananchi katika 
kushinda hiyo vita ambayo ni kubwa.
Akizungumzia
 redio alitaka watu wanaotumia vyombo hivyo kuangalia namna ya kutoachwa
 nyuma wakati huu wa mabadiliko makubwa ya teknolojia na sayansi ambapo 
matumizi ya mtandao ya utoaji wa habari papo hapo unaendelea.
Aliwataka
 watu kuzungumza nafasi ya radio katika kuleta maendeleo huku 
wakiangalia changamoto zinazoletwa na teknolojia ya habari.
Sherehe
 hizo ambazo ziliambatanishwa na midahalo kuhusu upashanaji wa vyombo 
vya habari na sheria iliwasilishwa na Mkurugenzi wa utangazaji wa TCRA 
Ntobi na pia watendaji wa UNDP kuhusu malengo ya maendeleo endelevu na 
namna radio inavyowezesha hamasa ya utekelezaji iliratibiwa na UNESCO.
Mkuu
 wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia
 Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini Zulmira Rodrigues alisema 
akimkaribisha Waziri Nape kwamba washiriki katika sekta ya utangazaji 
wanatakiwa kuwa pamoja ili kukuza upashanaji wa habari katika maeneo ya 
pembezoni.
Alishauri kuwepo na kuaminiana ili kufanikisha malengo  ya kuleta maendeleo kwa kupeana nafasi na kushirikishana.
Alitaka watanzania kutumia nguvu ya radio kukabiliana na matatizo mbalimbali ya kitaifa na kuleta maendeleo yanayotakiwa.
Kukiwa
 na vituo vya radio 44,000 duniani Mwakilishi huyo wa UNESCO alisema 
kwamba  radio bado ina maslahi makubwa kwa wananchi kutokana na kutoa 
sauti kwa wakazi ili  kukabiliana na changamoto zilizopo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni