RAIS DKT. MAGUFULI AMUAPISHA MKUU WA MAJESHI YA ULINZI YA TANZANIA (CDF) PAMOJA NA VIONGOZI WENGINE IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Jenerali Venance Mabeyo kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Tanzania, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Luteni Jenerali James Mwakibolwa kuwa Mnadhimu Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Kamishna Jenerali Juma Malewa kuwa Kamishna Jenerali wa Magereza, Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Luteni Jenerali Paul Meela kuwa Balozi nchini DRC Congo, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Balozi Samuel Shelukindo kuwa Balozi nchini Ufaransa, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Mkuu mpya wa Majeshi ya Ulinzi ya Tanzania Jenerali Venance Mabeyo mara baada ya tukio la uapisho lililofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein (wakwanza kushoto), Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wapili kulia pamoja na Mkuu mpya wa Majeshi ya Ulinzi ya Tanzania Jenerali Venance Mabeyo mara baada ya uapisho Ikulu jijini Dar es Salaam.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni