Kamishna wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi la Polisi,Nsato Marijani 
akiwasili katika eneo lilipo jengo la ghorofa ambalo ni makazi ya sakari
 lililoungua moto huku akiongozana na Mwenyeji wake Kamanda wa Polisi 
mkoa wa Kilimanjaro,Wilbroad Mutafungwa.
 Jengo
 la ghorof mbili ,makazi ya askari Polisi wa vikosi mbalimbali mjii 
Moshi liliungua moto sehemu ya juu na kueteketeza vyumba tisa pamoja na 
mali za asakri waliokuwa wakiishi katika vyumba hivyo.. 
 Kamishna
 Marijani akiangalia athari iliyotokana na moto katika jengo hilo 
ulioteketeza vyumba tisa zikiwmo samani za ndani na nguo za familia za 
askari hao. 
 Kamishna
 Marijani akizungumza na CPL Erick Mwantingo mmoja wa askari waliopoteza
 vitu vyote vya ndani katika tukio hilo la moto. 
 Kamishna
 Marijani akita pole kwa PC  Maswi ambaye pia amepoteza vitu vyote vya 
ndani zikiwemo nguo katika tukio la moto lililoteketeza sehemu ya juu ya
 jengo hilo. 
 Kamishna Marijani akimfariji  CPL,Simba baada ya kutembelea jengo hilo kujionea athari iliyotokana na moto huo.
 Kamishna
 Marinaji akimpa pole SGT Hashim baada ya kupoteza vitu vyote vya ndani 
pamoja na mavazi kufuatia moto ulioteketeza seheumu ya juu ya jengo 
hilo. 
 Kamanda
 wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro,Wilbroad Mutafungwa akimuongoza Kamishna 
Marijani kukagua maeneo mengine  ya jengo hilo ambalo linakumbwa na 
tukio la moto kwa mara ya pili sasa.
 Kamishna
 wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi la Polisi ,Nsato Marijani 
akisalimiana na baadhi ya viongozi pamoja na wageni waliofika kwa ajili 
ya kutoa pole kwa asakri waliounguliwa vitu katika jengo hilo. 
 Waliovalia
 kiraia ni askari Polisi waliofikwa na janga la kuunguliwa moto vitu vya
 ndani pamoja na mavazi wakionekana wenye huzuni. 
 Afisa
 Mnadhimu daraja la kwanza wa jeshi la Polisi mkoa wa Kilimanjaro,Koka 
Moita akizungumza wakati wa ukaribisho wa Kamishna wa Operesheni na 
Mafunzo ya Jeshi la Polisi,Nsato Marijani alipotembelea kambi ya polisi 
mjini Moshi. 
 Kamnada
 wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro,Kamishna Msaidizi Mwandamizi,Wilbroad 
Mutafungwa akitoa taarifa juu ya tukio la moto katika jengo la makazi ya
 askari Polisi. 
 Mkuu
 wa Shule ya Polisi,Kamandanti Matanga Mbushi akizungumza wakati wa 
kuzifariji familia za askari waliopoteza vitu vyao katika tukio la moto.
 
 Kamishna
 wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi la Polisi,Nsato Marijani akitoa 
salamu za pole kwa niaba ya Mkuu wa jeshi la Polisni nchini ,IGP Ernest 
Mangu kwa askari waliopoteza vitu vyao wakati wa tukio la moto 
lililoteketeza vyumba tisa katika makazi ya askari Polisi mjini Moshi. 
Na Mahmoud Ahmad Kilimanjaro.
JESHI
 la Polisi nchini limetangaza kuwahamisha askari tisa wa vikosi 
mbalimbali vya jeshi hilo waliopoteza mali zao wakati wa tukio la moto 
lililoteketeza vyumba tisa vya jengo la ghorofa mbili ambalo ni makazi 
ya askari.
Mbali
 na hatua hiyo jeshi hilo pia limetoa kiasi cha Sh Milioni tisa kwa 
familia za askari hao kwa ajili ya kuanza kununua vitu vidogo yakiwemo 
mavazi baada ya kutoambulia chochote wakati wa tukio hilo zikiwemo sare 
za jeshi hilo.
Kamishna
 wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi la Polisi,Nsato Marijani ametoa kauli
 hiyo jana kwa niaba ya Mkuu wa jeshi la Polisi ,Inspekta 
Jenerali,Ernest Mangu wakati akizifariji familia za askari hao pamoja na
 kutembelea jengo lililoteketea kujionea athari za moto huo uliotokea 
usiku wa kuamkia juzi.
Akiwasilisha
 salamu za Pole kwa niaba ya IGP Mangu,Kamishna Marijani alisema jeshi 
la Polisi litaendelea kutoa msaada kwa askari hao hadi pale maisha yao 
yatakaporejea huku akivishukuru vikosi vya jeshi la zima moto vya uwanja
 wa ndege wa KIA,kiwanda cha sukari cha TPC na Halmashauri kwa kazi 
waliyofanya.
Kamanda
 wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro Kamishna Msaidizi mwandamizi wa 
Polisi,Wilbroad Mutafungwa amemwelea kamishna Nsato kuwa thamani ya mali
 za askari zilizoteketea kwa moto imefikia sh Mil 93.9 huku akiomba 
wadau kujitokeza kusaidia familia hizo.
Tukio
 la moto katika jengo hilo lililopo jirani na ofisi za kikosi cha 
kutuliza ghasia lilitokea usiku wa kuamkia jana majira ya saa 2:30 usiku
 ,ukianzia katika chumba kimojawapo cha ghorofa ya pili na kuenea katika
 vyumba vingine nane wakati huo umeme ukiwa umekatika.
Kufuatia
 moto huo familia tisa za askari hao zenye jumla ya watu 40, ambao 23 ni
 watu wazima na 17 ni watoto tayari zimepatiwa malazi ya muda katika 
chuo cha Polisi Moshi wakati taratibu nyingine za kuwasaidia 
zikiendelea.
Tayari
 jeshi la Polisi mkoa wa Kilimanjaro limeunda timu ya wataalamu kutoka 
katika jeshi hilo wakisaidiana na wale wa kikosi cha zimamoto pamoja na 
shirika la umeme (TANESCO) kufanya uchunguzi wa matukio ya moto katika 
jengo hilo.
Mwisho.



 
 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni