Mwandishi Wetu,Arusha
  
Wasomi
  nchini wamepongeza uteuzi wa majaji wawili wanawake wa Mahakama ya Afrika na
  Haki za Binadamu(AfCHPR)uliofanywa na Wakuu wa Umoja wa Afrika(AU) katika mkutano
  wa 28 uliofanyika nchini Ethiopia kuwa unaelenga kujenga usawa wa kijinsia
  katika chombo hicho cha maamuzi.
  
 Mkutano huo pamoja na mambo mengine
  ulipitisha majina ya majaji wawili  ambao ni Jaji Bensaoula Chafika kutoka
  Algeria na Jaji Chizumila Rose Tujilane wa Malawi ambao wataitumikia mahakama
  hiyo kwa kipindi cha miaka sita ijayo.
  
Majaji
  hao wanachukua nafasi zilizoachwa wazi na Jaji Fatsah Ouguergouz(Algeria) na
  Jaji Duncan Tambala(Malawi)ambao utumishi wao ulikoma tangu Septemba  5,2016.
  
Mhadhiri
  Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Sebastian Kolowa Memorial(Sekomu),Dk Happiness
  Rwejuna aliyewaongoza wanafunzi wa sheria kutembelea Mahakama hiyo yenye
  makao yake jijini hapa alisema uamuzi uliofanywa na AU ni mzuri na ufaa
  kuigwa na nchi wanachama katika uteuzi wa wanawake wenye uwezo katika nafasi
  za maamuzi.
  
“Naamini
  idadi ya wanawake wenye elimu ya juu wapo wengi na wanaweza kufanya kazi kwa
  umahiri mkubwa,isihishie katika ngazi ya AU tuu bali ishuke hadi kwa nchi
  moja moja kuona wanawake wana mchango muhimu katika maendeleo ya Afrika kwa
  ujumla,”alisema
  
Majaji
  hao wanatarajiwa kuapishwa katika kikao cha 44 kinachotarajiwa kufanyika
  Machi 6,2017 jijini Arusha ikiwa ni mara ya kwanza kwa mahakama hiyo kuwa na
  majaji wanawake watano katika majaji 11 wa mahakama hiyo tangu ianze kazi
  zake mwaka 2004.
  
Naye
  Emmanuel Chipanta mwanafunzi wa mwaka tatu alisema uwepo wa mahakama hiyo una
  umuhimu katika kuimarisha utawala sheria kwani kumekua na makosa mengi
  yanayotendeka ambayo wahusika hawana budi kukabiliana na mkondo wa sheria.
  
Alisema
  uwiano wa kijinsia unatajwa katika itifaki iliyoanzisha mahakama hiyo katika
  ibara ya 12(2) na Ibara ya 14(3).
  
Kwa
  upande wake Mwanasheria wa Mahakama hiyo,Selemani Kinyunyu wakati akijibu
  hoja za wanafunzi hao waliotaka kufahamu uamuzi wan chi za Afrika kutaka
  kujiondoa katika Mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai alisema sula hilo
  lina sura mbili katika nchi zinazotaka kujiondoa na zinazotaka kubaki.
  
“Zipo
  nchi zinazoona mahakama hii imekua ikiwalenga viongozi wa Afrika zaidi badala
  ya kushughulikia jinai ulimwenguni kote hivyo kuona hamna sababu ya kuendelea
  kuwa mwanachama,laikini wapo wanaodhani ni muhimu kuendelea kuwepo ili kuotoa
  mapendekezo ya maboresho pale penye mapungufu jambo ninaloliunga mkono,”alisema



Hakuna maoni:
Chapisha Maoni