HARRISON FORD ANUSURIKA KUPATA AJALI YA NDEGE

Muigizaji filamu nyota Mmarekani, Harrison Ford, 74, amenusurika kupata ajali ya ndege aliyokuwa akiiendesha huko California, nchini Marekani.

Imeelezwa kuwa tukio hilo lilitokea pale alipopewa maelekezo ya kutua katika njia ya kutulia ndege katika uwanja wa ndege wa John Wayne uliopo kaunti ya Orange.

Hata hivyo Ford alitua vibaya katika njia ya ndege zilizopakiwa na kupitiliza karibu na ndege ya American Airlines iliyokuwa na abiria 110 na watumishi.
                Muigizaji filamu Harrison Ford akiangalia ndege yake baada ya kutua asipostahili

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni