Tume 
ya Taifa ya Uchaguzi imewatahadharisha watu wanaochukua kadi za kupigia 
kura za wenzao na kuzizuilia au kubaki nazo kuwa ni kinyume cha Sheria.
Hayo 
yamesema na Mkurugenzi wa Huduma za Kisheria wa Tume ya Taifa ya 
Uchaguzi Bw. Emmanuel Kawishe wakati akitoa elimu ya mpiga kura katika 
halmashauri ya manispaa ya Bukoba na Shinyanga hivi karibuni.
Alisema
 kifungu cha 88 cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi kinasema kuwa ni kosa la
 jinai kwa mtu kuchukua kadi ya mpiga kura mwingine na kuiziulia, 
kukataa kuirudisha au kubaki nayo kwa uzembe.
Bw. 
Kawishe alifafanua kuwa kumekuwa na malalamiko kwamba inapofikia karibu 
na kipindi cha uchaguzi, baadhi ya watu wanachukua kadi za wapiga kura 
wengine na kuzizuia kinyume cha Sheria.
Hata, 
hivyo alisema kutokana na kutoa elimu ya mpiga kura kupitia mikutano na 
kuhudhuria maonesho mbalimbali, baadhi ya wananchi wameelewa umuhimu wa 
kadi hizo na kuahidi kutoampa mtu kadi zao za kupigia kura.
“Kwa 
hiyo katika jambo hilo tumekuwa na mrejesho ambo ni chanya lakini 
tunachowaomba ukiandikishwa tunza kadi yako ya mpigia kura” alisema Bw. 
Kawishe na kuongeza kuwa;
“Jambo
 la pili mwananchi usikubali mtu achukue kadi yako ya mpigia kura na 
wala usitumie kadi yako ya mpiga kura kwenye kuchukulia dhamana sehemu 
yoyote”
“Kwa 
sababu itakwenda kuchukulia dhamana alafu utashindwa kwenda kupiga kura 
unapofika wakati wa kupiga kura, mwananchi ajue kwamba kupiga kura ni 
haki yake”
Alisema
 mtu aliyejiandikisha asipokwenda kupiga kura anakosa haki ya kuchagua 
kiongozi anayemtaka na badala yake anawaacha wenzako wakuchagulie 
kiongozi.
“Unaacha
 kupiga kura alafu baadaye anakuja kulalamika unasema huyu kiongozi 
simtaki kumbe kura moja inatosha kubadilisha matokeo ya eneo zima” 
alisema.
Hivyo 
aliwasihi wananchi waendelee kuzingatia amani katika uchaguzi na 
kuwashukuru kwa jinsi uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 na uchaguzi mdogo 
uliofanyika Januari 22 mwaka huu kwa jinsi ulivyokuwa na amani na 
utulivu.
”Kwa 
kweli Watanzania tutambue kuwa amani ni yetu sisi sote na sisi ndio 
tutakaoilinda hiyo amani tuiweke Tanzania yetu kwanza alafu sisi 
baadaye” aliwakumbusha Watanzania.
Akijibu
 swali la mmoja wa wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Bukoba aliyehoji 
anayepoteza kadi ya mpiga kura anachukuliwa hatua gani kumuwajibisha, 
Bw. Kawishe alisema hakuna hatua yoyote inayochukuliwa dhidi yake.
Alifafanua
 kuwa wale wote wanaopoteza kadi ya mpiga kura wanatakiwa wafike kwenye 
kituo cha uboreshaji wa daftari la wapiga kura na kujieleza na 
watapatiwa kadi nyingine.
Mwenyekiti
 wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji (R) Semistocles Kaijage (kulia) 
akisalimiana namwenyeji wake Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania 
Kanda ya Shinyanga Jaji Richard Kibelabaada ya mwenyeji wake kumpokea 
wakati akiwasilimkoaniShinyanya kutoa Elimu ya Mpiga Kura 
mkoanihumo.Kushoto niNaibuMsajili wa MahakamaKuu kanda ya Shinyanga 
Sekela Mwaiseje.
Mkurugenzi
 waHuduma za Kisheria wa Tume ya Tiafa ya Uchaguzi Bw. Emmanuel Kawishe,
 akisamiliana na Mkurugenzi wa Halamashauri ya Manispaa ya ShinyangaBw. 
Geofrey Ramadhani Mwangulumbi baada ya kuwasili kwenye Halmashauri hiyo 
kutoa Elimu ya Mpiga kura.
Mkurugenzi
 waHuduma za Kisheria wa Tume ya Tiafa ya Uchaguzi Bw. Emmanuel Kawishe,
 akizungumza na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Josephine Matirowakati 
alipomtembeleaofisinikwakemkoanihumo.
Mkurugenzi
 waHudumaza Kisheria wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bw. Emmanuel 
Kawisheakitoa Elimu ya Mpiga kurakupitia Kituo cha redioFarajaFm cha 
mkoaniShinyangamwishonimwa wiki hii.Kuliakwake ni mtangazaji wa redio 
hiyo FaustinKasala.
Mkurugenzi
 wa Huduma za Kisheria wa Tume ya Tiafa ya Uchaguzi Bw. Emmanuel 
Kawishe, akitoa Elimu ya Mpiga kura kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari 
ya Old Shinyangailiyopomanispaaya Shinyanga.Pichana Hussein Makame, NEC.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni