Vodacom yazindua simu mpya ya Smart Bomba
·        Matumizi  yake yapo kwenye lugha ya Kiswahili
·        Inauzwa ikiwa imeunganishwa na kifurushi cha intanenti  chenye GB 30 za buree kwa miezi 3!
Dar
 es Salaam,Jumatano Februari 03,2017:Sasa ni wakati wa watanzania 
kufurahia ubunifu wa kiteknolojia wa mawasiliano unaoendana sambamba na 
mazingira yao halisi na kufurahia kupata taarifa na burudani kwa njia ya
 interneti ambapo kuanzia leo wateja wa Vodacom,mtandao unaoongoza 
nchini wataweza kujipatia simu za kisasa zinazotumia interneti aina ya 
Smart Bomba.
Simu
 za Smart Bomba ambazo zimezinduliwa rasmi nchini  leo zinapatikana kwa 
gharama nafuu ya shilingi 99,000/-muundo wa matumizi yake uko katika 
lugha ya taifa ya Kiswahili pia zinanunuliwa zikiwa tayari 
zimeunganishwa na kifurushi cha interneti  chenye GB 10 za buree kwa 
mwezi na ofa hii inatolewa katika kipindi cha miezi 3 mfululizo kwa 
ajili ya kumuwezesha mteja kupata na kufurahia intanenti yenye kasi 
kubwa ya Vodacom  mahali popote na wakati wowote.
Mbali
 na muundo wa matumizi ya simu hii kuwa katika lugha ya Kiswahili na 
kwendana  na mazingira halisi ya maisha ya watanzania walio wengi,simu 
za Smart Bomba zina umbo la kuvutia,nyepesi na zina kioo cha mbele,cha 
ukubwa wa kutosha,zinafanya kazi kwa kutumia teknolojia ya android 
inaongeza kasi ya kuperuzi internet,inayo kamera ya kurekodi na kupiga 
picha kwa kiwango chenye ubora wa hali ya juu vilevile inao mfumo wa 
utambuzi wa ramani ya maeneo mbalimbali ujulikanao kama GPS ambao unatoa
 maelekezo kuonyesha mahali mtu alipo na mahali aendapo kwa urahisi 
hususani madereva wa teksi ambao huwapeleka wateja wao sehemu mbalimbali
 wasiozijua,na zimeunganishwa na program za simu za kurahisisha Maisha 
za Vodacom kama vile M-Paper.
Akiongea
 wakati wa  uzinduzi wa simu hii,Mkuu wa Masoko wa Vodacom Tanzania 
kanda ya Dar es Salaam,Domician Mkama,alisema wakati ni huu wa kila 
mtanzania kuweza kufurahia matumizi ya simu za kisasa zinazotumia 
internet (Smart Phones) kwa ajili ya kupata taarifa na burudani kutoka 
mitandaoni kutokana na kupatikana kwa mara ya kwanza kwa gharama nafuu 
nchini.
“Kuingia
 sokoni kwa simu za Smart Bomba za gharama nafuu na zilizotengenezwa 
kwendana sambamba na mazingira na Maisha ya watanzania walio wengi 
zikiwa zimeunganishwa na GB 30 kwa matumizi ya miezi 3 ya mwanzoni ni 
ofa ya kipekee ambayo imebuniwa kubadilisha maisha ya wateja wetu  walio
 wengi na kuendelea kuyafanya kuwa murua”.
Mkama
 aliongeza kusema “Hivi sasa tuko katika zama za kidigitali ambayo 
mawasiliano ya watu wengi yanafanyika kupitia mitandao ya kijamii ,hivyo
 wananchi wengi wakiwa na simu za kisasa zinazotumia internet wanaweza 
kufanya mambo mengi kwa urahisi na haraka kuanzua kwenye biashara,kupata
 taarifa mbalimbali,kutumiana salamu na kupata burudani za muziki na 
sinema kutoka mitandaoni”.Alisema.
Alisema
 wakati ni huu kwa makundi mbalimbali ya watanzania katika jamii 
kuchangamkia fursa hii pekee kwa kununua simu ya Smart Bomba kwa gharama
 nafuu na kuwa mtu wa kisasa anayeenda na wakati na simu hizi zinatukuwa
 zinapatikana kwenye maduka yote yanayouza simu nchini na zina waranti 
ya mwaka mmoja.
Kwa
 kutambua kuwa kundi kubwa kwenye jamii linahitaji matumizi ya intanenti
 kupata burudani  na kupakua muziki hususani muziki wa Bongo 
Flava,uzinduzi wa simu hii na matangazo yake yamemuhusisha mwanamuzi  
nguli wa  Bongo Fleva nchini,  Diamond Platnumz.
Akiongea
 wakati wa uzinduzi huo,Diamond Platnumz aliwapongeza Vodacom kwa 
kuingiza sokoni simu ya kisasa ya Smart Bomba ambayo imelenga kutumiwa 
na wananchi wengi  kwa kuwa ina unafuu na inaendana na Maisha halisi ya 
watanzania. “Sasa ni wakati wa kila mtanzania kwenda kidigitali kwa ku 
chart,kupata nyimbo za wazipendazo live kupitia simu zao na kupakua 
filamu wazipendazo ,kutumiana salamu na picha kwa njia ya simu,kuperuzi 
internet na kupata taarifa na burudani kupitia ncha za vidole vyao na 
haya yote yanapatikana katika mtandao mkubwa nchini wa Vodacom pekee.
 Mkuu wa Mauzo na Usambazaji wa Vodacom Tanzania,kanda ya Dar es Salaam, Domician Mkama(kushoto) akimshuhudia Balozi
 wa kampuni hiyo,Mwanamuziki nguli wa kimataifa,Nasibu Abdul” Diamond 
Platinumz” akiongea na wakazi wa Kariakoo jiji la Dar es Salaam leo na 
waandishi wa habari(hawapo pichani) wakati wa Uzinduzi wa simu mpya aina
 ya Smart Bomba yenye matumizi ya lugha ya Kiswahili inayopatikana kwa 
shilingi 99,000/-tu iliyoambatanishwa na kifurushi chenye intanenti ya 
GB 10 za buree kwa kipindi cha miezi 3. 
 Balozi
 wa Vodacom Tanzania,Mwanamuziki nguli wa kimataifa,Nasibu Abdul” 
Diamond Platinumz” akiongea na wakazi wa Kariakoo jiji la Dar es Salaam 
leo wakati wa Uzinduzi wa simu mpya aina ya Smart
 Bomba yenye matumizi ya lugha ya Kiswahili inayopatikana kwa shilingi 
99,000/-tu iliyoambatanishwa na kifurushi cha intanenti chenye GB 10 za 
buree kwa kipindi cha miezi 3. Kulia ni Mkuu wa Mauzo na Usambazaji wa 
Vodacom Tanzania,kanda ya Dar es Salaam, Domician Mkama.
Balozi
 wa Vodacom Tanzania,Mwanamuziki nguli wa kimataifa,Nasibu Abdul” 
Diamond Platinumz” akiwaburudisha wakazi wa Kariakoo jiji la Dar es 
Salaam leo wakati wa Uzinduzi wa simu mpya aina ya Smart Bomba yenye 
matumizi ya lugha ya Kiswahili inayopatikana kwa shilingi 99,000/-tu 
iliyoambatanishwa na kifurushi cha intanenti chenye GB 10 za buree kwa 
kipindi cha miezi 3.




Hakuna maoni:
Chapisha Maoni