HOFU YA BOMU YASABABISHA NDEGE YA UTURUKI KUTUA CANADA

Ndege ya Shirika la Ndege la Uturuki iliyokuwa ikitokea New York imelazimishwa kwenda Canada baada ya tishio la bomu.

Maafisa wamesema ndege hiyo iliyokuwa na abiria 256 ilitua salama katika uwanja wa Kimataifa wa Halifax mashariki mwa Canada.

Polisi nchini Canada wanaendelea na uchunguzi, hata hivyo hawakuelezea lolote juu ya tishio hilo la bomu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni