POLISI MISRI WAMEPATA MIILI YA WAHAMIAJI 15 WA AFRIKA WALIOUWAWA KWA RIASI

Polisi nchini Misri wamepata miili ya wahamiaji 15 wa Afrika ambao inaonekana walipigwa risasi na kufa kaskazini mwa Penisula ya Sinai.

Pia wahamiaji wanane wamepatikana hai lakini wamejeruhiwa. Haijafahamika kuwa nani alilishambulia kundi hilo karibu na mji wa Rafah mpakani mwa Gaza.

Kumekuwa na hali ya hofo katika eneo hilo, ambalo jeshi la Misri linapambana wanamgambo wa kundi la Dola ya Kiislam (IS).

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni