RAIS UHURU KENYATTA AFANYA MABADILIKO YA BARAZA LAKE LA MAWAZIRI KENYA

Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya ametangaza kufanya mabadiliko ya baraza lake la mawaziri na kufanya mabadiliko ya muundo wa serikali yak e kufuatia kugubikwa na rushwa.

Katika mabadiliko hayo aliyoyafanya baada ya mawaziri sita kujiuzulu kwa tuhuma za rushwa rais Kenyatta pia ameongeza wizara kutoka 19 na kuwa 20 idara za serikali kutoka 26 hadi 41 ili kuongeza ufanisi.

Katika mabadiliko hayo rais Uhuru Kenyatta amewatimua kazi mawaziri watano ambao walisimamishwa kazi kutokana na kukabiliwa na tuhuma za rushwa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni