UFARANSA YAWASAKA WAPIGANAJI WA IS WALIONUSURIKA KATIKA TUKIO LA PARIS

Msako mkali unaendelea wa kutafuta wafuasi wa kundi la Dola ya Kiislam (IS) walionusurika wakati wa mashambulizi ya kigaidi siku ya Ijumaa yaliyouwa watu 129 Jijini Paris nchini Ufaransa.

Polisi wamemtaja Salah Abdeslam, mwenye umri wa miaka 26, kuwa ni mtuhumiwa muhimu, ambaye alisimamishwa na polisi siku ya mashambulizi na kuachiliwa aende.

Wakati huo huo ndege za kivita za Ufaransa zimeshambulia ngome kuu ya kundi la Dola ya Kiislma nchini Syria.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni