Katibu
 wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na waandishi wa habari
 nje ya ukumbi wa NEC ,CCM Makao Makuu Dodoma akiwa ameshikilia kitabu 
cha Kanuni za Kamati ya Wabunge Wote wa Chama Cha Mapinduzi. 
Kamati
 Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM katika kikao chake cha siku moja
 kilichofanyika leo Novemba 15, 2015 mjini Dodoma imewateua wana-CCM 
watatu watakaopigiwa kura na wabunge wote wa CCM ili kumpata mgombea wa 
CCM katika nafasi ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Walioteuliwa
 kugombea nafasi hiyo na Kamati Kuu iliyofanyika chini ya Mwenyekiti wa 
CCM, Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ni pamoja na Naibu Spika 
aliyemaliza muda wake Ndugu JOB NDUGAI, Dkt. TULIA ACKSON na Ndugu 
ABDULAH MWINYI.
 
Kwa
 upande wa Naibu Spika wa Bunge, mchakato wa kuchukua fomu kwa wabunge 
wa CCM wanaoomba ridhaa kugombea nafasi hiyo utaanza kesho Novemba 16, 
2015 na kukamilika Novemba 17, 2015 saa kumi kamili jioni.
 
Wana-CCM
 hao watatu watapigiwa kura na Kikao cha Kamati ya Wabunge wote wa CCM 
kitakachofanyika kesho Novemba 16, 2015 saa nne asubuhi katika ofisi za 
Makao Makuu ya CCM Dodoma ilikuchagua jina moja kugombea nafasi hiyo 
katika Bunge la Jamhuri ya Muungano.
 
Kuhusu
 nafasi ya Naibu Spika, alisema kulikuwa na kasoro za kutofuata kanuni 
za chama ambapo hadi jana ni mwanachama mmoja tu ndiye
 aliyekuwa amechukua fomu ya kugombea ambaye ni Mbunge wa Ilala, Mussa Azzan ‘Zungu,’ lakini atatakiwa kuchukua fomu upya.
 
“Ibara
 ya 57, Kanuni za kamati ya wabunge wote wa CCM toleo la 2010 toleo la 
nne 2011, mbunge yeyote anayetaka kugombea nafasi ya Naibu Spika 
atatakiwa kuchukua fomu kupitia kamati hiyo na atairudisha kisha kamati
 itakaa kupata jina moja,” alisema Nape.
 
Kwa
 mujibu wa maelezo hayo mbunge wa chama hicho anayetaka kugombea Unaibu 
Spika, atatakiwa kuchukua fomu leo Novemba 16, kwa ada ya Sh
 100,000 kisha atairudisha kesho Novemba 17, ndipo kamati itakaa kuchambua na kupitisha jina moja.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni