Mkuu
 wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini toka Ofisi ya Rais Menejimenti ya
 Utumishi wa Umma Bw. Florence Temba akiwaeleza waandishi wa habari 
(Hawapo pichani) kuhusu utaratibu wa Serikali kutumia TEHAMA katika 
kufanya mikutano kwa kutumia mfumo wa Mawasiliano ya  (Video  
comference) ambapo kikao kimoja kitawaunganisha pamoja washiriki kutoka 
 Mikoa 8 ambapo mada huwasilishwa na kutoa fursa ya kuwasiliana moja kwa
 moja (interactivity) kwa maswali na ufafanuzi leo jijini Dar es salaam.
 Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Habari (MAELEZO) Bi Zamaradi 
Kawawa.
Mkurugenzi
 Msaidizi  wa Idara ya Habari  (MAELEZO) Bi Zamaradi Kawawa  akifafanua 
jambo kwa waandishi wa Habari (hawapo pichani) wakati wa mkutano kati ya
 Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na vyombo vya habari 
uliofanyika leo jijini Dar es asalam.Kulia kwake ni Mkuu wa Kitengo cha 
Mawasiliano Serikalini toka Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa 
Umma Bw. Florence Temba na Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini toka Ofisi ya
 Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Priscus Kiwango.
Baadhi
 ya waandishi wa habari wakifuatilia mkutano wa Ofisi ya Rais 
Menejimenti ya Utumishi  kuhusu utaratibu wa Serikali kutumia TEHAMA 
katika kufanya mikutano ambapo mfumo wa Mawasiliano ya (Video 
comference)  utatumika ili kupunguza gharama za mikutano kwa Taasisi za 
Serikali.
Mkuu
 wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini toka Ofisi ya Rais Menejimenti ya
 Utumishi wa Umma Bw. Florence Temba akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa 
Habari kuhusu faida za kutumia TEHAMA ikiwemo kuokoa fedha zilizokuwa 
zinatumika awali kuandaa mikutano hiyo ambapo kwa sasa washiriki 
watashiriki mikutano hiyo wakiwa katika vituo vyao vya kazi leo jijini 
Dar es salaam. Kulia ni Mkurugenzi wa TEHAMA Serikalini toka Ofisi ya 
Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Priscus Kiwango. 
                                                                            (Picha na Frank Mvungi-Maelezo) 
 
                                                                            Na Jovina Bujulu-MAELEZO 
Uanzishaji
 wa matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) Serikalini 
utaboresha na kuongeza ufanisi wenye tija ambao utapunguza gharama za 
utendaji na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi. 
Kupitia 
utaratibu huu wa vikao kazi ambavyo vitaendeshwa kwa kutumia mfumo wa 
mawasiliano ya video ambapo kikao kimoja kitaunganisha kwa pamoja 
washiriki kutoka mikoa nane ambapo mada huwasilishwa na kutoa fursa ya 
kuwasiliana moja kwa moja kwa maswali na ufafanuzi. 
 
Hayo
 yamesemwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Rais 
Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Florence Temba alipokuwa akiongea na
 waandishi wa habari kuhusu matumizi ya TEHAMA katika kupunguza gharama 
za uendeshaji vikao kazi.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni