NIKO INSURANCE LIMITED YABADILI JINA NA KUWA SANLAM GENERAL INSURENCE


Afisa Mtendaji Mkuu wa iliyokuwa NIKO Insurance Bw. Manasseh Kawoloka akizungumza mbele ya wageni waalikwa waliohudhuria hafla ya kubadilisha jina la kampuni hiyo ambapo sasa inaitwa Sanlam General Insurance.hafla hiyo ilifanyika katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam.
Kampuni ya Bima Niko Insurance limited Imebadili jina na kuwa Sanlam General Insurance Limited.Mabadiliko hayo yanalenga Kupanua Wigo Na kuimarisha uwepo wake Nchini Tanzania na Afrika Mashariki kwa Jumla.Sanlam General Insurance Itaendelea Kutoa Huduma Mbalimbali za Bima Kwa Wateja Binafsi na Mashirika Nchini Tanzania.Huduma za Sanlam General Insuarance ni Pamoja na za Biashara na Binafsi kama vile Magari,Moto Na Nyinginezo.
Afisa Mwandamizi wa Ukuaji wa Mashirika wa Sanlam Emerging Markets (SEM) Ndugu Manasseh Kawaloka Akitoa Hotuba yake Kwenye halfa ya Kampuni ya NIKO Insuarance Limited Ilipobadili Jina na kuwa Sanlam General Insurance.Sanlam General Insurance Yenye Makao Makuu yake Nchini Afrika KusiniInamiliki 46%ya Hisa za Niko.Kupitia Kampuni yake Tanzu ya Masoko yanayokua yaani Sanlam Emerging Markerts..
Picha ya Viongozi wa Kampuni ya Sanlan Pamoja na NIKO Insurance wakiwa wameshikana mikono Mara baada ya Uzinduzi wa Sanlam General Insuarence.
Afisa Mwandamizi wa Ukuaji wa Mashirika wa Sanlam Emerging Markets (SEM) Alisema Kuwa Sanlam Group ni Kampuni yenye Sifa Kubwa,Hivyo Mabadiliko ya NIKO Insurance Kuwa Sanlam General Insurance Utaleta Ufanisi wa Hali ya Juu Pamoja Utendaji wa Kibiashara Kwa Kampuni Hiyo.Akieleza zaidi alisema Watanzania sasa watapata nafasi zaidi ya Kupata Aina mbalimbali za Bidhaa za Bima Zenye ubunifu kufidia Majanga Binafsi na ya Kibiashara .
Kampuni ya Iliyobadili Jina Sanlam General Insurance Inatoa Huduma Mbalimbali za Bima Katika Wigo Mpana Kwa Wateja Binafsi Pamoja na Mashirika Nchini Tanzania .Huduma Zitolewazo na Kampuni ya Bima ya Sanlam General Insurance Zinalenga Biashara na Watu Binafsi Kama Magari ,Moto ,Uhandisi pamoja na Bima Maalum.Kabla ya Kubadili Jina Kampuni ya NIKO Insurance Imekuwa Ikitoa Huduma Nchini Tangu Mwaka 2005.
Mjumbe wa Bodi ya Sanlam General Insurance (zamani NIKO Insurance)Ndugu Josep Mungai Akitoa Hotuba yake wakati wa Uzinduzi huo.
Mabadiliko ya NIKO Insurance Limited kuwa Sanlam General Insurance Yanafuatia Mabadiliko ya Kampuni ya African Life Assuarence ya Tanzania na Kuwa Sanlam Life Insurance.Sanlam General Insurance Inatoa utaalamu na Uzoefu wa Hali ya Juu kwa Wateja wake Pamoja na Wadua wengine wanaofanya kazi na Kampuni hiyo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni