Benki
 ya Amana leo hii imehitimisha wiki ya huduma kwa wateja ambapo katika 
tawi la Mwanza mkurugenzi wa benki hiyo <b>Dk Muhsin Masoud alitoa
 zawadi mbali mbali kwa wateja wenye sifa tofauti tofauti kama 
ioneshavyo pichani.
Mkurugenzi
 huyo alikutana na wateja mbali mbali tawini  hapo ili 
kubadilishana nao mawazo na pia kupokea maoni toka kwao katika kuboresha
 huduma kwa wateja wa benki hiyo pekee ya Ki Islamu nchini.
Kilele
 hicho cha wiki ya huduma kwa wateja kimefanyika katika matawi yote ya 
benki hiyo ambayo kwa Dar es Salaam ni Tandamti, Lumumba, Nyerere na 
Main, vile vile Arusha na Mwanza.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni