MONABAN ANZA KAMPENI MTU KWA MTU LEVOLOSI



Mollel ameyasema hayo wakati alipokuwa akijitambulisha na kuomba kura kwa wakazi wa kata ya Levolosi na kuwataka kuendelea kukiamini chama cha mapinduzi pamoja na yeye kwani anatosha kuliongoza jimbo la Arusha Mjini.
Alisema kuwa anaomba kura kwa wanachama na wasiokuwa wanachama kwani maendeleo hayana itikadi za vyama vya siasa hivyo akawataka kumtuma naye awe mtumishi wa wananchi wa jimbo la Arusha mjini

“Mnajua siendi kuganga njaa bungeni bali naenda kupeleka kero zenu na nani uchungu na maendeleo ya kinamama,wazee na vijana kwani nitaanzisha saccos kwa kila kata ilimpate mikopo ya kujikwamua na kuweza kujiletea maendeleo”alisema Mollel.

Aliwataka wakereketwa na wale wafuasi wa vyama vingine kuweka pembeni ushabiki na kumchagua yeye ilikuirudiisha Arusha kuwa Giniva ya Afrika na kuirudisha Arusha yenye amani na kuweza kurudisha sifa ya jiji hilo.

Awali akimkaribisha Mgombea kwa wanachama na wafuasi wa chama hicho sanjari na wananchi Mwenyekiti wa chama hicho wilaya ya Arusha Dkta Wilfred ole Soiley amewakata kuacha ushabiki wa kisiasa na kumchagua Mollel kwani anatosha kuongoza jimbo la Arusha.

Soiley alisema kuwa pamoja na kupigwa katika uchaguzi mkuu kwa nafasi za udiwani mda umefika kwani uchaguzi ulipita na sasa ni wakati wa kuunganisha nguvu na kumpa kura za kishindo mgombea wa chama hicho.

“Nawasihi nduguzangu kutafuta wanachama kumi kwa kila mtu 
ilikuunganisha nguvu na kuipa ccm ubunge wa jimbo letu kwani nyinyi ni mashahidi wakubwa hakuna kilichofanyika kwa mda wa mbunge aliyemaliza mda wake kwa kipindi cha miaka mitano”alisema Soiley.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni