Kamishna
 wa Bajeti kutoka Wizara Fedha Bw. John Cheyo akitoa ufafanuzi kwa 
waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kuhusu taarifa za 
upotoshaji zilizoripotiwa na vyombo vya habari hapa nchini kuwa hazina 
yakauka, taarifa hizo ni za upotoshaji kwani mfumo wa Serikali wa bajeti
 unaiwezesha Serikali kupanga vipaumbele vya matumizi kulingana na 
bajeti ilivyopangwa ambapo fedha zinazokusanywa kupitia mfuko mkuu wa 
Serikali ndizo hutumika. Kushoto ni Kamishna msaidizi wa Bajeti Bw. 
Immanuel Tutuba na kulia ni Mkurugenzi msaidizi Idara ya habari Maelezo 
Bw. Vicent Tiganya.
Kamishna
 wa Bajeti kutoka Wizara Fedha Bw. John Cheyo akizungumza na waandishi 
wa habari leo jijini Dar es salaam kuhusu kubadilishwa kwa matumizi ya 
Fedha za Serikali ambazo zitaelekezwa kwenye shughuli zitakazowagusa 
wananchi ikiwemo uboreshaji wa sekta ya elimu ambapo awali fedha hizo 
zilipangwa kutumika katika sherehe za Uhuru na shughuli zisizo za 
lazima. Kulia ni Mkurugenzi msaidizi Idara ya Habari. (MAELEZO) Bw. 
Vicent Tiganya.
Kamishna
 msaidizi wa Bajeti Bw.Immanuel Tutuba akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa
 habari kuhusu namna Serikali inavyokusanya mapato yake na kuyaingiza 
katika mfuko mkuu wa Serikali ili yaweze kutumika katika utekelezaji wa 
bajeti ya Serikali. Kulia kwake ni Kamishna wa Bajeti Bw. John Cheyo na 
kushoto ni msemaji wa Wizara ya Fedha Bi. Ingiahedi Mduma.
Baadhi
 ya Waandishi wa Habari wakifuatilia mkutano wa Wizara ya Fedha na 
vyombo vya habari ambapo Kamishna wa Bajeti kutoka Wizara hiyo Bw. John 
Cheyo alitoa ufafanuzi kuhusu utekelezaji wa bajeti ya Serikali 
kulingana na mipango iliyowekwa katika kuwahudumia wananchi.
Kamishna
 msaidizi wa Bajeti Bw.Immanuel Tutuba akisisitiza jambo kwa waandishi 
wa habari leo jijini Dar es salaam .Kulia nia Msemaji wa Wizara ya Fedha
 Bi. Ingiahedi Mduma. (Picha na frank Mvungi- Maelezo) 
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni