RAILA ODINGA ASHINIKIZA MAWAZIRI ZAIDI WAJIUZULU KWA KASHFA ZA RUSHWA

Kiongozi wa Upinzani nchini Kenya Raila Odinga amepongeza uamuzi wa kujiuzulu kwa Waziri wa Wizara ya Ugatuaji Bi. Anne Waiguru kufuatia wizara yake kukumbwa na kashfa za ufisadi.

Hata hivyo Raila amemtaka Rais Uhuru Kenyatta kuwafukuza kazi mawaziri wengine ambao wizara zao zimekabiliwa na tuhuma za rushwa.

Aidha, Raila amesema amechanganyikiwa, labda Waiguru na rais Uhuru Kenyatta wampatie maelezo kutokana na kauli ya waziri huyo kudai afya yake sio nzuri na atamuomba rais ampagie kazi rahisi, ambapo amesema angependa kujua kazi hiyo rahisi ni ipi hata kama ni ya jikoni.
                 Anne Waiguru Waziri aliyejiuzulu wadhifa katika Wizara ya Ugatuaji

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni