Vijana
 wa YAM ( Youth Action Movement) ambao ni waandaaji wa tamasha hili 
linalofanyika kila mwezi wakionesha igizo lao lililobeba ujumbe unaosema
 ni jukumu la wazazi kuwaelimisha vijana juu ya afya ya uzazi na ujinsia
 ili kuwakinga na maambukizi ya VVU mimba katika umri mdogo na ngono 
katika umri mdogo.
Mwenyekiti
 wa UMATI dar es salaam Mr.Harith Shomvi ambae alikuwa mgeni rasmi 
 katika tamasha hilo akihutubia wananchi na kuwasisitiza wapate huduma 
za uzazi wa mpango na upimaji ambazo zilikuwa zikitolewa bure katika 
tamasha hilo. Tamasha hilo lilikuwa na kauli mbiu isemayo "JE kutoa 
 elimu  juu ya afya ya uzazi na ujinsia kwa vijana ni jukumu la nani?
 Baadhi ya
 wananchi wakijiandikisha ili waweze kupata huduma ya upimaji VVU na 
uzazi wa mpango zilizokuwa zikitolewa bure na UMATI katika tamasha hilo 
la jamvi la vijana.
 Mtoa huduma wan UMATI Bibi. Neema Orgeness akimpima mteja VVU.
 Mtoa
 huduma wa UMATI Monika Nkwera akimpatia mama huduma ya uzazi wa mpango 
wakati wa Tamasha la Vijana lililofanyika jijini Dar es Salaam mapema 
wikiendi hii. Tamasha hilo lilikuwa na kauli mbiu isemayo "JE kutoa 
 elimu  juu ya afya ya uzazi na ujinsia kwa vijana ni jukumu la nani?
Kikundi
 cha nyota kutoka Temeke wakionesha igizo linaloelezea umuhimu wa wazazi
 kuwapa elimu ya afya ya uzazi na ujinsia watoto wao ili kuwaepusha na 
ngono katika umri mdogo,mimba katika umri mdogo,VVU/UKIMWI,na pia athari
 zingine zitokanazo na ukosefu wa elimu na habari sahihi kuhusu afya ya 
uzazi na ujinsia.
Picha na Maelezo.







Hakuna maoni:
Chapisha Maoni