Meneja
 wa mipango  wa kapeni ya Binti Thamani Rosemacy Njoki   akizungumza na 
waandishi wa habari  (hawapo pichani) juu ya kampeni ya  kuwahamasisha 
wasichana kupenda kujiunga  na vyuo vya ufundi  ili kujifunza ufundi 
stadi  na kujiendeleza kimaisha  ikiwa ni pamoja na kujipatia ajira 
endelevu, amesema hayo katika kutano uliofanyika leo jijini Dar es 
Salaam. Kushotoni Mkuu wa Chuo cha ufundi cha Don Bosco Dodoma Fromac 
Mulu.
 Mratibu wa kampeni ya Binti Thamani wa taasisi ya Don Bosco, Agnes Mgongo, kisisitiza jambo katika mkutano uliofanyika leo jijini Dar es Salaam, kushoto ni Mkufunzi wa Chuo cha Ufundi cha Don Bosco   Jose Kaippan.
 Waandishi wa habari wakimsikiliza Meneja wa mipango  wa kapeni Binti Thamani Rosemacy Njoki
 Wafanyakazi wa Taasisi ya Don Bosco wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa chuo cha ufundi cha Don Bosco.
Picha na Emmanuel Massaka, Globu ya Jamii.
TAASISI
  ya kidini ya Don Bosco imeandaa kampeni ya  kuwahamasisha wasichana 
kupenda kujiunga  na vyuo vya ufundi  ili kujifunza ufundi stadi  na 
kujiendeleza kimaisha  ikiwa ni pamoja na kujipatia ajira endelevu.
Akizungumza jijini Dar es Salaam  Meneja wa mipango  wa kapeni ya Binti Thamani, Rosemacy Njoki amesema
 wana vyuo mbalimbali hapa nchini ambavyo vinatoa mafunzo ya ufundi 
stadi kwa vijana lakini  kumekuwa na asilimia ndogo ya vijana wakike 
wanaojiunga na mafunzo ya ufundi stadi ukilinganisha na idadi ya vijana 
wa kiume kwa mwaka.
amesema
 baadhi ya kozi zinazotolewa  na vyuo vya Don Bosco vilivyopo Dar es 
Salaam Dodoma na Iringa  ni ufundi Seremala, uchongaji vipuri,  uungaji 
na uundaji  vyuma, umeme wa viwandani na majumbani, uhazili, ujenzi, 
ufundi bomba na magari, ufundi cherehani uchapishaji na kompyuta.
Kampeni
 ya Binti thamani ni mwendelezo wa uhamasishaji kwa wasichana kuibua na 
kutatua changamoto mbalimbali za vijana hususani wasichana kutambua kuwa
 kuna fursa ya kujiendeleza na kufanikiwa kupitia mafunzo ya ufundi 
baada ya kumaliza mafunzo yao.
Kampeni hiyo itasaidia kuwakumbusha kuwa wasichana nao wana uwezo wa kufanya kazi yoyote hasa anapokuwa na malengo chanya.
Kampeni
 hiyo leo itawakutanisha wasichana mbalimbali hasa wanafunzi wa shule za
 sekondari wapatao 1000 katika mikoa wa Dar es Salaam.
“Lengo
 la kampeni hii ni kuwakutanisha wasichana na wadau mbalimbali 
waliopitia mafunzo ya ufundi stadi na kuwahimiza  kuwa mabalozi wazuri 
katika kuhakikisha wasichana wengi Zaidi wanapenda mafunzo ya ufundi 
stadi.
“Tunawaomba
 wazazi  na walezi tusaidiane kwa pamoja katika harakati za 
kuwahamasisha wasichana kwani ndio tegemeo la jamii yetu,”  Rosemacy.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni