TAASISI YA DON BOSCO YAHAMASISHA WASICHANA KUPENDA KUJIUNGA NA VYUO VYAO

 Meneja wa mipango  wa kapeni ya Binti Thamani Rosemacy Njoki   akizungumza na waandishi wa habari  (hawapo pichani) juu ya kampeni ya  kuwahamasisha wasichana kupenda kujiunga  na vyuo vya ufundi  ili kujifunza ufundi stadi  na kujiendeleza kimaisha  ikiwa ni pamoja na kujipatia ajira endelevu, amesema hayo katika kutano uliofanyika leo jijini Dar es Salaam. Kushotoni Mkuu wa Chuo cha ufundi cha Don Bosco Dodoma Fromac Mulu.
 Mratibu wa kampeni ya Binti Thamani wa taasisi ya Don Bosco, Agnes Mgongo, kisisitiza jambo katika mkutano uliofanyika leo jijini Dar es Salaam, kushoto ni Mkufunzi wa Chuo cha Ufundi cha Don Bosco   Jose Kaippan.
 Waandishi wa habari wakimsikiliza Meneja wa mipango  wa kapeni Binti Thamani Rosemacy Njoki
 Wafanyakazi wa Taasisi ya Don Bosco wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa chuo cha ufundi cha Don Bosco.
Picha na Emmanuel Massaka, Globu ya Jamii.
TAASISI  ya kidini ya Don Bosco imeandaa kampeni ya  kuwahamasisha wasichana kupenda kujiunga  na vyuo vya ufundi  ili kujifunza ufundi stadi  na kujiendeleza kimaisha  ikiwa ni pamoja na kujipatia ajira endelevu.
Akizungumza jijini Dar es Salaam  Meneja wa mipango  wa kapeni ya Binti Thamani, Rosemacy Njoki amesema wana vyuo mbalimbali hapa nchini ambavyo vinatoa mafunzo ya ufundi stadi kwa vijana lakini  kumekuwa na asilimia ndogo ya vijana wakike wanaojiunga na mafunzo ya ufundi stadi ukilinganisha na idadi ya vijana wa kiume kwa mwaka.
amesema baadhi ya kozi zinazotolewa  na vyuo vya Don Bosco vilivyopo Dar es Salaam Dodoma na Iringa  ni ufundi Seremala, uchongaji vipuri,  uungaji na uundaji  vyuma, umeme wa viwandani na majumbani, uhazili, ujenzi, ufundi bomba na magari, ufundi cherehani uchapishaji na kompyuta.
Kampeni ya Binti thamani ni mwendelezo wa uhamasishaji kwa wasichana kuibua na kutatua changamoto mbalimbali za vijana hususani wasichana kutambua kuwa kuna fursa ya kujiendeleza na kufanikiwa kupitia mafunzo ya ufundi baada ya kumaliza mafunzo yao.

Kampeni hiyo itasaidia kuwakumbusha kuwa wasichana nao wana uwezo wa kufanya kazi yoyote hasa anapokuwa na malengo chanya.
Kampeni hiyo leo itawakutanisha wasichana mbalimbali hasa wanafunzi wa shule za sekondari wapatao 1000 katika mikoa wa Dar es Salaam.

“Lengo la kampeni hii ni kuwakutanisha wasichana na wadau mbalimbali waliopitia mafunzo ya ufundi stadi na kuwahimiza  kuwa mabalozi wazuri katika kuhakikisha wasichana wengi Zaidi wanapenda mafunzo ya ufundi stadi.

“Tunawaomba wazazi  na walezi tusaidiane kwa pamoja katika harakati za kuwahamasisha wasichana kwani ndio tegemeo la jamii yetu,”  Rosemacy.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni