WANAWAKE WA IRELAND WAMTUMIA SIKU ZAO ZA HEDHI WAZIRI MKUU

Wanawake nchini Ireland wamekuwa wakimtumia ujumbe wa twitta Waziri Mkuu wao Enda Kenny unaoelezea siku zao za hedhi, katika kuonyesha hasira zao dhidi ya sheria kali za kuzuia utoaji mimba.

Mchekeshaji Grainne Maguire ndiye alianza kumtumia ujumbe wa aina hiyo Waziri Mkuu Kenny siku ya jumatatu katika kutaka kuondolewa kifungu cha nane cha mabadiliko ya Katiba ya Ireland.

Mabadiliko ya Katiba ya kifungu hicho yanaruhusu kuokoa maisha ya mama pale tu ujauzito utakapotishia uhai wa mjamzito na ni kosa kisheria kutoa mimba.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni