Dr
 Adelhelm James Meru akimkabidhi Flaviana Matata barua ya kuchaguliwa 
kwake huku  kaimu Mkurugenzi Devota Mdachi akishuhudia, katika ofisi za 
wizara hiyo
 
Mwanamitindo wa Kimataifa anaefanyia 
kazi zake za nchini Marekani Flaviana Matata amechagulia na Wizara ya 
Maliasili   kuwa Balozi wa Hiyari 'Good Will Ambassador' kwa kipindi cha
 miaka mitatu kwa dhumuni la kutangaza  vivutio vya utalii vya Tanzania 
ndani na nje ya nchi.
Flaviana ambaye juzi alikuwa mmoja kati
 ya shuhuda wa kushuhudia wizara ya maliasili na utalii wakizindua rasmi
 tangazo litakalokuwa linatangaza vivutio vya Tanzania nje ya anchi 
alitawazwa leo hii na katibu mkuu Dr Adelhelm James Meru aliyemkabidhi 
kwa niaba ya Waziri , Mheshimiwa Lazaro Nyalandu huku Kaimu Mkurugenzi 
Madam Devota Mdachi akishuhudia.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni