MAENDELEO ENDELEVU 17 YA DUNIA YAZINDULIWA TANZANIA
Mratibu
 wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi Mkazi wa UNDP Bw. Alvaro
 Rodriguez (kulia) na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la
 UN Women nchini Tanzania, Anna Collins-Falk (katikati) wakipata picha 
ya kumbukumbu sambamba na mmoja wa wadau wa maendeleo. (Picha na Zainul 
Mzige wa Modewjiblog).
Na Mwandishi wetu
UMOJA wa Mataifa kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania wamezindua rasmi malengo ya Maendeleo Endelevu 17 ( SDGs).
Malengo
 hayo ambayo pia yanajulikana kama malengo ya dunia yamezinduliwa jana 
Septemba 29 katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam.
Uzinduzi
 huo ulifanywa na Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi
 Mkazi wa UNDP Bw. Alvaro Rodriguez, Kamishina wa mipango (POPC) Bw. 
Paul Kessy, na Kamishina wa Mipango wa Zanzibar, Bw. Ahmed Makame kwa 
niaba ya serikali, Bi. Fionnuala Gilsenan, Balozi wa Ireland na Bi. Liz 
Lloyd, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered Tanzania kwa 
niaba ya wadau wa mradi wa Project Everyone Partners.
SDGs
 ni wito wa dunia wa kuchukuliwa kwa hatua za kuufuta umaskini, kuihami 
dunia dhidi ya uharibifu wa mazingira na kuhakikisha kwamba kila 
mwanadamu anaishi maisha stahiki katika amani na ustawi.
Katika
 malengo hayo 17 yapo makusudio 169 yanayotoa ramani ya utengenezaji wa 
sera za maendeleo na namna ya kutekeleza kwa miaka 15 ijayo.
Malengo
 hayo yakijengwa juu ya mafanikio ya malengo ya milenia (MDGs), 
yameingiza vitu vipya kama mapambano dhidi ya tofauti za kiuchumi, 
ubunifu, mabadiliko ya tabia nchi, lishe, amani na haki. SDGs ni mpango 
wa dunia unaojikita kwa ustawi wa wanancni na dunia.
Mkurugenzi
 Mkazi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Awa Dabo (kushoto) na Kiongozi wa
 mabalozi wa nchi za nje hapa nchini Mheshimiwa Juma Mpango, ambaye ni 
balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) wakiwa wameshikilia 
lengo namba 16 na 17 kati ya malengo 17 ya Maendeleo Endelevu ya Dunia 
ambayo yamezinduliwa rasmi nchini Tanzania jana 29, Septemba 2015.
Akizungumza
 umuhimu wa malengo hayo, Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa 
nchini na Mwakilishi wa UNDP Bw. Alvaro Rodriguez amesema: “Kwa mara ya 
kwanza katika historia ya dunia , serikali zimekutana na kukubaliana 
kupeana malengo kwa ajili ya kila mtu. Malengo haya yatasaidia mataifa 
yote kushirikiana katika kuwezesha ustawi, kupunguza matumizi na 
kuilinda dunia dhidi ya mabadiliko ya tabia nchi.Katika hilo 
watashughulikia elementi zinazohusu maendeleo endelevu: ukuaji wa 
uchumi, ustawi wa jamii na kulinda mazingira.”
Akizungumzia malengo hayo Bw. Paul Kessy amesema kwamba serikali ya Tanzania ipo tayari kwa malengo hayo.
Alisema
 kwamba Rais Jakaya Kikwete alikuwa New York, Marekani kwa ajili ya 
kutia saini malengo hayo na hilo linaonesha ni kiasi gani serikali ya 
Tanzania iko tayari kushirikiana na wadau wengine kuufuta umaskini.
Pia
 alisema:“Wakati huu, masuala ya uimarishaji wa muundo wa utekelezaji na
 kuamsha upya ushirikiano wa kidunia katika maendeleo ni msingi mzuri”
Naye
 Kamishina wa mipango wa Zanzibar, Bw Ahmed Makame : “Nikiangalia 
malengo haya 17 ya SDGs, ninafuraha kuona kwamba Zanzibar imekuwa sehemu
 ya mchakato huu...”.
Ofisa
 Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered Tanzania, Bi. Liz Lloyd 
akipozi kwa picha na lengo na tisa kabla ya uzinduzi rasmi wa Malengo ya
 Dunia kwa Maendeleo Endelevu.
Aidha alisema kwamba Tanzania imeanza vyema katika utekelezaji wa malengo hayo.
Alisema
 kwa kuangalia uzoefu uliopatikana katika malengo ya milenia, inaonekana
 namna bora ya kuuoanisha malengo ya kitaifa na ya dunia.
Ninafurahi
 kusema kwamba Zanzibar tuko katika mchakato wa kutengeneza mkakati wa 
maendeleo wa kitaifa na tumepanga kufikia malengo ya SDGs.
Akisisitiza
 umuhimu wa ushirikiano katika kufanikisha maendeleo, Bi.Fionnuala 
Gilsenan, amesema taifa lake Ireland lipo tayari kusaidia kufanikisha 
malengo ya maendeleo endelevu.
“Malengo
 ya dunia yaliyojengwa katika Malengo ya Milenia yamelenga kukabiliana 
na matatizo ya zamani kwa mbinu mpya. Zimelenga kukabiliana na tatizo la
 umaskini na ukosefu wa usawa katika masuala ya uchumi. SDGs haiwezi 
kufanikiwa bila kuyaangalia masuala ya mabadiliko ya tabia nchi, usawa 
wa jinsia, haki za biandamu na kukabiliana na mfumo inayobagua.”
Akizungumza
 kwa niaba ya wadau wa Project Everyone, Bi. Liz Lloyd alielezea umuhimu
 wa sekta binafsi kushirikiana na Umoja wa Mataifa na serikali ya 
Tanzania katika kusambaza ujumbe wa malengo ya dunia.
Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO), nchini Tanzania, Dk.Rufaro Chatora akipozi la lengo namba 3.
“Kama
 benki huwa tunazungumza na umuhimu wa kuendelea kuwapo. Huu si tu msemo
 bali ahadi tunayoishi nayo kila siku. Malengo ya Dunia yanatoa nafasi 
adhimu ya ushirikiano na taasisi kubwa duniani, kutekeleza malengo 17 
kwa nia ya kufufua ushirikiano wa dunia kwa maendeleo endelevu.
Standard
 Chartered inajisikia furaha ya kuwa nchini Tanzania kwa miaka mingi na 
inatumaini kwamba kwa ushirikiano huu kila mtu anayeishi nchini hapa 
atafaidika na maendeleo endelevu ya kiuchumi na kijamii.”
Malengo
 ya Maendeleo Endelevu yalizinduliwa Septemba 25 wakati viongozi wa 
dunia walipokutana pamoja mjini New York. Malengo haya yataanza kutumika
 Januari 1,2016.
Mkuu wa ushauri wa ufundi wa Mfuko wa Umoja wa mataifa wa Ukuzaji Mitaji (UNCDF), Peter Malika akipozi na lengo na 17.
Mratibu
 wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi Mkazi wa UNDP Bw. Alvaro
 Rodriguez katika picha ya pamoja na baadhi ya wageni waalikwa kabla ya 
uzinduzi rasmi wa malengo hayo nchini Tanzania.
Mtaalam
 wa mawasiliano kutoka UNFPA, Sawiche Wamunza (kushoto) sambamba na 
Afisa Habari wa kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Usia 
Nkhoma Ledama katika picha ya ukumbusho.
Meza
 kuu katika halfa ya uzinduzi wa malengo ya Maendeleo Endelevu 17 ( 
SDGs) nchini Tanzania, kutoka kushoto ni Mtaalamu wa masuala ya uchumi 
wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Dar es salaam, Rogers
 Dhliwayo, Balozi wa Ireland nchini Tanzania, Mh. Fionnuala Gilsenan, 
Kamishina wa mipango (POPC) Bw. Paul Kessy, Mratibu wa Mashirika ya 
Umoja wa Mataifa na Mwakilishi Mkazi wa UNDP Bw. Alvaro Rodriguez, 
Kamishina wa Mipango wa Zanzibar, Bw. Ahmed Makame pamoja na Ofisa 
Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered Tanzania, Bi. Liz Lloyd.
Mratibu
 wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi Mkazi wa UNDP Bw. Alvaro
 Rodriguez, akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa malengo ya Maendeleo
 Endelevu 17 ( SDGs).
Ofisa
 Mtendaji Mkuu wa Benki ya Standard Chartered Tanzania, Bi. Liz Lloyd 
akielezea ushiriki wa benki yake katika utekelezaji wa malengo ya 
Maendeleo Endelevu 17 ( SDGs).
Kamishina
 wa mipango (POPC) Bw. Paul Kessy akizungumza kwa niaba ya serikali ya 
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye hafla ya uzinduzi wa malengo ya 
Maendeleo Endelevu 17 ( SDGs).
Kamishina wa Mipango wa Zanzibar, Bw. Ahmed Makame akiwakilisha serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Balozi
 wa Ireland nchini Tanzania, Mh. Fionnuala Gilsenan akizungumza kwenye 
hafla hiyo ambapo alisisitiza umuhimu wa ushirikiano katika kufanikisha 
maendeleo.
Baadhi
 ya wadau wa maendeleo kutoka mashirika na balozi mbalimbali 
waliohudhuria uzinduzi wa malengo ya Maendeleo Endelevu 17 ( SDGs) 
iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Baadhi
 ya wageni waalikwa na wakuu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini 
Tanzania wakifuatilia maoni na maswali yaliyokuwa yakiwasilishwa kwenye 
hafla hiyo.
Mmoja wa wawakilishi wa vijana akiuliza swali meza kuu.
Mwakilishi
 Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi Duniani 
(UNHCR), Joyce Mends-Cole akijibu moja ya swali lililoulizwa na kijana 
(hayupo pichani).
Sehemu ya wadau wa Maendeleo, taasisi mbalimbali, asasi za kiraia, waandishi wa habari waliohudhuria uzinduzi huo.
Mwakilishi
 wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya watu duniani 
(UNFPA), Dkt. Natalia Kanem akifafanua jambo katika kipindi cha maswali 
na majibu.
Mratibu
 wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi Mkazi wa UNDP Bw. Alvaro
 Rodriguez (kulia), Kamishina wa Mipango wa Zanzibar, Bw. Ahmed Makame (
 wa pili kulia), Balozi wa Ireland nchini Tanzania, Mh. Fionnuala 
Gilsenan (kushoto) Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya 
Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahaya (wa pili kushoto) kwa 
pamoja wakifunua pazia maaluma kuashiria uzinduzi rasmi wa malengo ya 
Maendeleo Endelevu 17 ( SDGs).
Sasa yamezinduliwa rasmi.
Shamra shamra za uzinduzi zikiendelea.
Fataki zikisherehesha uzinduzi wa malengo ya Maendeleo Endelevu 17 ( SDGs).
Baadhi
 ya wanafunzi wa shule ya msingi Uhuru mchangayiko na wadau mbalimbali 
wa maendeleo, waandishi wa habari wakiwa kwenye picha ya pamoja na vibao
 vya malengo ya Maendeleo Endelevu 17 ( SDGs).
Meza
 kuu katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi 
Uhuru mchangayiko walioshiriki kutengeneza tangazo maalum la kuelimisha 
jamii kuhusiana na malengo ya Maendeleo Endelevu 17 ( SDGs).
Meza
 kuu katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa mashirika ya 
Umoja wa Mataifa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Meza
 kuu katika picha ya pamoja na baadhi ya waandishi wa habari akiwemo 
Mwanahabari mkongwe Mama Eda Sanga walioshiriki kwenye uzinduzi huo.
Bendera ya Umoja wa Mataifa, SDG's na bendera za nchi mbalimbali zikipepea kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni