VIJANA 435,225 WANAISHI NA MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI NCHINI KENYA

Baraza la Taifa la Kudhibiti Ukimwi nchini Kenya (NACC) limesema vijana 435,225 wenye umri wa kuanzia miaka 10 hadi 19 wanamaambukizi ya Ukimwi, huku wengine 119,899 wakiwa na virusi vya ugonjwa huo lakini bado hawajatambuliwa.

Kwa mujibu wa baraza hilo kutokana na idadi hiyo ya maambukizi ya Ukimwi, vijana 7,500 walifariki dunia kwa ugonjwa huo mwaka jana nchini Kenya kutokana na kucheleweshewa matibabu pamoja na kunyanyapaliwa mno.

Ripoti ya NACC inaonyesha kuwa kaunti ya Nairobi inaongoza kwa kuwa na vijana 49,904 wenye kuishi na maambukizi ya Ukimwi, Homa bay ya pili vijana 46,530 ikifuatiwa na Kisumu ikiwa na vijana 37,110 walioathirika na Ukimwi, Siaya vijana 33,810 huku Marsabit ikiwa na vijana 450, Tana River 360 na Wajiri ya mwisho ikiwa na vijana 150 waathirika wa Ukimwi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni