Mmiliki na Mkurugenzi
 Mtendaji wa Kampuni ya Black Sensation, Lilliane Masuka (katikati), 
akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo 
asubuhi, kuhusu Tamasha la Fahari ya Mwafrika litakalofanyika viwanja 
vya Club ya Escape One, Oktoba 3, 2015 Mikocheni jijini Dar es Salaam. 
Kushoto ni Mkurugenzi wa Uendeshaji wa kampuni hiyo, Gabriel Manyaga na 
Mkurugenzi wa Ubunifu wa kampuni hiyo, Charlotte Mwaigwisya. 
 Mkurugenzi
 wa Uendeshaji wa Kampuni ya Black Sensation, Gabriel Manyaga (kushoto),
 akizungumza katika mkutano huo. Kulia ni Mmiliki na  Mkurugenzi 
Mtendaji wa kampuni hiyo, Lilliane Masuka. 
 Mkurugenzi wa Ubunifu wa kampuni hiyo, Charlotte Mwaigwisya akitoa ufafanuzi kwa waaandishi wa habari kuhusu tamasha hilo.
 Wanahabari kutoka vyombo mbalimbali wakichukua taarifa hiyo.
Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
Na Dotto Mwaibale
KAMPUNI
 ya Black Sensation inatarajia kufanya tamasha lenye kutangaza utamaduni
 wa Mwafrika Oktoba 3 mwaka huu katika Club ya Escape One iliyopo 
Mikocheni Jijini Dar es Salaam ambalo linatambulika  kama 'Fahari ya 
Mwafrika'.
Akizungumza
 katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo Mmiliki na 
Mkurugenzi Mtendaji wa  Kampuni hiyo, Liliane Masuka alisema tamasha 
hilo ni la muhimu katika kuutangaza utamaduni wetu.
Masuka
 alisema tamasha hilo linatarajiwa kuonyesha vitu mbalimbali vya asili 
ya mwafrika na tamaduni zake litakuwa la aina yake kutokana na 
maandalizi pamoja na washiriki.
Mkurugenzi
 huyo alisema tamasha hilo litakuwa na lengo lake likiwa ni kuhamasisha 
utamaduni na kubadilishana kimawazo pamoja na kufanya maonesha ta 
tamaduni mbalimbali.
"Oktoba
 3 mwaka huu tutakuwa na tamasha ambalo litatambulika kwa jina la 
'Fahari ya Mwafrika' na tunatarajia kutakuwepo na vikundi mbalimbali 
ambavyo vitaonesha utamaduni wetu," alisema. 
Masuka
 alisema katika tamasha hilo kutakuwepo na muziki wa dansi, vichekesho, 
maigizo, ngoma na vitu mbalimbali ambavyo kwa pamoja vinatangaza 
utamaduni wa Tanzania.
Alisema
 pia kutakuwa na vikundi mbalimbali kutoka shule za Sekondari, 
wanamitindo na wabunifu wa ndani ambao wataonesha vitu vyenye kuakisi 
utamaduni wa Tanzania na Afrika kwa ujumla.
Mkurugenzi
 wa Uendeshaji wa kampuni hiyo, Gabriel Manyaga alisema pamoja na kuanda
 tamasha hilo pia wanatarajia kutoa tuzo za Fahari ya Afrika kwa watu 
ambao wataonesha kuudumisha uafrika kupitia tamasha hilo kubwa na la 
aina yake.
Alisema
 tuzo zitatolewa kwa kushirikiana na vyombo mbalimbali ambavyo kwa 
pamoja vitazingatia sifa husika na sio kuchaguana kishabiki kama tuzo 
zingine zinazotolewa.
Manyaga
 alisema wao kama Black Sensation wanaamini kuwa wataweza kukuza na 
kuibua vipaji vya wasanii wa hapa nchini ambao wameshindwa kuonekana na 
kutambulika kutokana na sababu ambazo ziko nje ya uwezo wao.
Mkurugenzi
 wa Ubunifu wa Kampuni hiyo, Charlotte Mwaigwisya alisema kampuni hiyo 
ilibuni tamasha hilo ili kutoa fursa ya kuutangaza utamaduni wetu ambao 
kwa kiasi kikubwa umeanza kusahulika kutoka na sababu mbalimbali ikiwemo
 kupungua kwa kasi ya kuutangaza.
 (Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com 
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni